056-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Waaqi’ah Aayah 75-82: فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

056-Al-Waaqi’ah: Aayah: 75-82

 

 

Kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 

فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ ﴿٧٥﴾

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota.

 

 

وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ ﴿٧٦﴾

Na hakika hicho ni kiapo adhimu lau mngelijua.

 

 

إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ ﴿٧٧﴾

Hakika hii bila shaka ni Qur-aan tukufu.

 

 

فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ ﴿٧٨﴾

Katika Kitabu kilichohifadhiwa.

 

 

لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ ﴿٧٩﴾

Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa.

 

 

تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٨٠﴾

Ni uteremsho kutoka kwa Rabb wa walimwengu.

 

 

أَفَبِهَـٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ ﴿٨١﴾

Je, kwa maneno haya nyinyi ni wenye kuikanusha na kuibeza?

 

 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha.

 

 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha. [Al-Waaqi’ah: 75-82]

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

 

عن ابْنِ عَبَّاسٍ، قَالَ مُطِرَ النَّاسُ عَلَى عَهْدِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ أَصْبَحَ مِنَ النَّاسِ شَاكِرٌ وَمِنْهُمْ كَافِرٌ قَالُوا هَذِهِ رَحْمَةُ اللَّهِ ‏.‏ وَقَالَ بَعْضُهُمْ لَقَدْ صَدَقَ نَوْءُ كَذَا وَكَذَا ‏"‏ ‏.‏ قَالَ فَنَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: ((‏فَلاَ أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ‏))‏ حَتَّى بَلَغَ ‏ ((وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ‏))

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) kwamba kulitokea mvua zama za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ambapo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alisema: “Baadhi ya watu wamepambukiwa asubuhi wakiwa wenye kushukuru, na wengineo wenye kukufuru (kukosa shukurani kwa Allaah).” Walioshukuru walisema: “Hii ni Rahmah ya Allaah.” Na wale waliokufuru walisema: “Nyota kadhaa na kadhaa zimesadikisha.” Hapo ikateremka Aayah hii:

فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ ﴿٧٥﴾

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota.

 

Mpaka kufikia:

 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha. [Al-Waaqi’ah: 75-82]

 

[Muslim Kitaabul-Iymaan, Mlango wa Kubainisha Kufru Kwa Anayesema Tumenyeshewa Mvua Kutokana Na Nyota]

 

 

Share