17-Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan Kwa Mwenye Hedhi Au Nifaas Akiangalia Mswahafuni

 

Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan Kwa Mwenye Hedhi Au Nifaas Akiangalia Mswahafuni

 

Fataawaa Mas-ala 60 Kuhusu Hedhi Na Nifaas

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI:

 

Nini hukumu ya usomaji wa Qur-aan kwa mwenye hedhi na nifaas akiwa anaangalia Mswahafuni au anahifadhi na haswa tukizingatia katika hali ya dharura kuwa ni mwanafunzi au mwalimu?

 

JIBU:

 

 

Si vibaya kwa mwanamke mwenye hedhi na nifaas kusoma Qur-aan kwa haja kama vile yeye ni mwalimu au mwanafunzi ambaye anasoma uradi wake wa siku kama ni usiku au mchana. Ama usomaji wa Qur-aan kwa maana ya usomaji wa kupata ujira na thawabu asifanye kwa sababu ‘Ulaama wengi wanaona kuwa mwenye hedhi haimfali kusoma Qur-aan.

 

Share