02-Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Akinunua Mnyama Wa Udhwhiyah Kisha Akapata Maradhi Achinjwe

 

Akinunua Mnyama Wa Udhwhiyah Kisha Akapata Maradhi Achinjwe

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

 

Atakayenunua kichinjwa na kumchunga kisha akapata maradhi au kuvunjika mguu wake je, huchinjwa?

 

JIBU:

 

 

Atakayeainisha kichinjwa na kusema: “Hiki ndicho kichinjwa changu huwa ndio kichinjwa.”

 

a-Akipatwa na maradhi au kuvunjika na ikiwa wewe ndiye uliyesababisha basi hatochinjwa na yapasa kununua mbadala wake au kilicho bora zaidi.

 

b-Na ikiwa wewe hukusababisha basi atafaa.

 

 

[Majmuw’ Al-Fataawaa (25/99)]

 

 

Share