49-Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Amehirimia ‘Umrah Akapatwa Hedhi Na Mahram Wake Ilibidi Asafari

 

 

Fataawaa Mas-ala 60 Kuhusu Hedhi Na Nifaas

 

49-Amehirimia ‘Umrah Akapatwa Hedhi Na Mahram Wake Ilibidi Asafari

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI:

 

Mwanamke alipohirimia ‘Umrah alipofika Makkah akapatwa na hedhi na mahram wake akatakiwa asafiri haraka na hana mtu mwengine Makkah ni nini hukumu yake?

 

 

JIBU:

 

Anatakiwa asafiri naye akiwa pamoja na ihraam yake  kisha atarejea akitwaharika ikiwa mtu huyu anaishi Saudi Arabia kwani kurudi kwake kutakua wepesi  kwa sababu hahitajii passport au mfano wake. Ama akiwa ni mgeni na kurudi kwake ni kwa taabu basi itabidi atufu na kufanya Sa’y na kupunguza nywele  na kumaliza ‘Umrah yake katika safari hiyo hiyo ya awali, kwani Twawaaf yake wakati huo itakuwa ni jambo la dharura na dharura huhalalisha yaliyokatazwa.

 

 

Share