13-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Unyenyekevu Wake: Akiomba Kuishi Umasikini Na Kufishwa Pamoja Na Masikini Na Akinasihi Kuwa Karibu Nao

 

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

13-Akiomba Kuishi Umasikini Na Kufishwa Pamoja Na Masikini

Na Akinasihi Kuwa Karibu Nao

 

www.alhidaaya.com

 

عَنْ أَنَسٍ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏"‏ اللَّهُمَّ أَحْيِنِي مِسْكِينًا وَأَمِتْنِي مِسْكِينًا وَاحْشُرْنِي فِي زُمْرَةِ الْمَسَاكِينِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ‏"‏ ‏.‏ فَقَالَتْ عَائِشَةُ لِمَ يَا رَسُولَ اللَّهِ قَالَ ‏"‏ إِنَّهُمْ يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ قَبْلَ أَغْنِيَائِهِمْ بِأَرْبَعِينَ خَرِيفًا يَا عَائِشَةُ لاَ تَرُدِّي الْمِسْكِينَ وَلَوْ بِشِقِّ تَمْرَةٍ يَا عَائِشَةُ أَحِبِّي الْمَسَاكِينَ وَقَرِّبِيهِمْ فَإِنَّ اللَّهَ يُقَرِّبُكِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ‏"‏

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameomba: ((Ee Allaah Nijaalia uhai wa umaskini na nifishe nikiwa maskini na nifufue pamoja na kundi la masaakini Siku ya Qiyaamah)).  ‘Aaishah akasema: “Kwa nini ee Rasuli wa Allaah?”  Akasema: ((Hakika wao wataingia Jannah kabla ya matajiri kwa miaka arubaini. Ee ‘Aaishah usimrudishe maskini (bila kumpa kitu, umpe) hata kipande cha tende. Ee ‘Aaishah kurubiana nao kwani Allaah Atakukurubisha Siku ya Qiyaamah)) [At-Tirmidhiy]

 

Share