20-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Unyenyekevu Wake: Akimhudumia Yeyote Aliyemuomba Njiani

 

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

20-Unyenyekevu Wake Akimhudumia Yeyote Aliyemuomba Njiani

www.alhidaaya.com

 

 

 

  عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ أَنَّ امْرَأَةً لَقِيَتِ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي طَرِيقٍ مِنْ طُرُقِ الْمَدِينَةِ فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اللَّهِ إِنَّ لِي إِلَيْكَ حَاجَةً؟ قَالَ: يَا أُمَّ فُلَانٍ اجْلِسِي فِي أَيِّ نَوَاحِي السِّكَكِ شِئْتِ أَجْلِسْ إِلَيْكِ، قَالَ: فَقَعَدَتْ فَقَعَدَ إِلَيْهَا رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ حَتَّى قَضَتْ حَاجَتَهَا  

Kutoka kwa Anas bin Maalik (رضي الله عنه) kwamba mwanamke mmoja alikutana na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika njia mojawapo ya Madiynah akasema: Ee Rasuli wa Allaah, hakika mimi nnakuhitaji jambo. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Akasema:  “Ee Ummu fulani, kaa kitako upande wowote ule wa njia nami nitakaa pamoja nawe.”  Anas akasema:  Akakaa kitakao, naye Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akakaa kitako (akamsikiliza) hadi akamtimizia haja yake.” [Abuu Daawuwd, ameisahihisha Al-Albaaniy  - Swahiyh Abiy Daawuwd (4818),  Swahiyh Al-Jaami’ (7857)]

 

 

Share