Biskuti Za Ufuta Na Jam

Biskuti Za Ufuta Na Jam

 

Vipimo

 

Unga vikombe 2

Sukari ya kusaga   1/4 Kikombe

Siagi  250 gms

Jam  kisia

Ufuta kisia

Vanilla 1 kijiko cha chai

 

Namna Ya  Kutayarisha Na Kupika

  1. Tia kwenye mashine ya kusaga (blender) au mashine ya keki, siagi, yai, sukari na vanilla uchanganye hadi ichanganyike vizuri.
  2. Tia baking powder, na unga na changanya kwa mkono vizuri.
  3. Paka siagi sinia ya kupikia ya oveni.
  4. Tengeneza viduara vidogo vidogo.
  5. Bonyeza kila kiduara katikati kwa kidole, kisha weka jam, halafu juu yake paka mayai na unynyuzie ufuta.
  6. Pika katika moto wa chini 350ºF kwa muda wa dakika 20-25.
  7. Tayari kwa kuliwa.

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

 

 

Share