19-Abu Bakr Asw-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu 'anhu): Alipotoka Kwenda Sokoni

Siku ya pili baada ya kuwa Khaliyfah wa Waislamu, Abu Bakr (Radhiya Allaahu ‘anhu) alitoka kuelekea sokoni huku akiwa amebeba rundu la nguo.

'Umar bin Khataab na Abu 'Ubaydah (Radhiya Allaahu ‘anhu) walipomwona katika hali hiyo wakamuuliza;

"Unakwenda wapi ewe Khaliyfah wa Mtume wa Allaah?"

Akawajibu;

"Naelekea sokoni".

'Umar akamuuliza;

"Unakwenda kufanya nini sokoni na umepewa u-Khaliyfah juu ya Waislamu?"

Abu Bakr akajibu;

"Wanangu nitawalisha nini?"

'Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) akatoa akasema;

"Itakuwa bora kama tutashauriana na Maswahaba wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) waweze kumjaalia Khaliyfah wa Waislamu malipo maalum ili aweze kujihusisha na matatizo ya Ummah".

Maswahaba wote wakakubali ushauri huo.

 

Share