06-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Nia na usia wa kurejesha haki

 
 
Nia na usia wa kurejesha haki:
 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “ Sio haki kwa Muislamu ambae zitampita siku mbili na ana kitu anataka kuusia ila usia ule utakuwa umeandikwa kichwani mwake.” Baada ya kusikia hadithi hii Umar bin Khatab akasema, ‘ Haikunipitia mimi hata siku moja baada ya kusikia hadithi hii ila nilikuwa tayari nimeshatayarisha usia wangu.’ (Bukhari na Muslim)
 
Ikiwa mja ni mdaiwa na hana mali ya kulipa deni hilo ni juu yake aweke nia ya kulipa deni hilo na akokoteze kwa kumuomba Mwenyezi Mungu amsaidie alilipe deni hilo na aandike usia kwa jamaa zake kumlipia deni hili.
Share