07-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kinachotakiwa kiwepo katika usia:

 
Kinachotakiwa kiwepo katika usia:
 
Katika masiku haya ambayo sheria imekuwa inavunjwa na haifuatwi hali kadhalika ujahili kuenea kila upande na elimu ya dini kuwa ni chache yampasa Muislamu ausie katika yale mambo ambayo yatamkosha yeye kwanza na kufuatwa isivyo, hili litamuokoa na wengine kumfuata katika makosa haswa katika mambo yanayohusu mauti, swala ya jeneza na mambo yenye kuhusiana nayo, hivyo anatakiwa ausie kufuatwa kwa sunna na kuacha bid’a, maasi na chochote kilichozushwa katika dini katika mambo hayo; kama vile kuomboleza kwa sauti na makelele, kujipiga, na kuomba maombi ya kijahili. Ni juu ya mwenye kuusia ausie kukataza mambo haya na ajiepushe nayo na awahadharishe jamaa zake na ubaya na uovu wake.
 
Wakati fulani Abu Musa aliugua na kuhisi maumivu makubwa, kwa maumivu hayo akazimia ilhali kichwa chake kipo chini ya uangalizi wa mwanamke mmoja katika jamaa zake, mwanamke yule baada ya kuona hali ya Abu Musa akapiga kelele kwa nguvu lakini Abu Musa hakuweza kusema kitu kwa hali aliyokuwa nayo, baada ya kuzindukana akasema, ‘Mimi najikosha kwa yale aliyojikosha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) kwani Mtume alijikosha na haya yafuatayo (hakuyataka kabisa yatokee): As-Swaliqah; yaani mtu mwenye kunyanyua sauti yake kwa juu wakati wa msiba, na Al-Haaliqah; mwenye kunyoa nywele zake wakati wa msiba na Ash-Shhaqah; anayerarua na kuchana nguo zake wakati wa kuomboleza.” (Bukhari na Muslim)
 
Ni juu ya wasia unaotolewa kuhusu mali na vitu uzingatie kwanza kulipa madeni au amuusie katika wale ambao hawarithi theluthi katika mali yake kwa sharti kuwa isipatikane madhara katika kuusia huko.
Share