09-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Hakuna kuusiwa mali mwenye kurithi

 
 
Hakuna kuusiwa mali mwenye kurithi:
 
 
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala) ameshatoa haki kwa kila mwenye kurithi nasibu yake, kama vile tunavyojifunza hayo katika surat Nisaa na sura nyinginezo. Haifai kuzidisha au kupunguza kile alichoweka Mwenyezi Mungu katika sheria yake tukufu, hivyo basi mwenye kutaka atoe usia basi na atoe kwa wale ambao hawarithi kisheria.
 
 Imethibiti kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “ Mwenyezi Mungu amempa kila mwenye haki haki yake anayostahiki hivyo hausiwi (mali) mwenye kurithi.” (Abu Daud)
 
Share