14-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kauli ya Mwisho ya Mtu kuwa ni Laa ilaha illa llahi

 
Kauli ya Mwisho ya Mtu kuwa ni Laa ilaha illa llahi :
 
 
Mja atakapohisi sakaraatul maut na kukaribia mwisho wake katika maisha haya ya dunia basi na ahudhurishe katika moyo wake hisia hizo na aelekee kwa Mola wake akiwa na mapenzi na khofu kwake na akithirishe kauli ya ‘Laa ilaha illa llah’ ili ahitimishe itikadi yake kwa kauli hiyo ya Tawhid.
 
Watu wote watakaokuwa karibu yake katika hali hiyo ya sakaraatul maut wamkumbushe hilo na wamwambie aliseme kwa upole ili Mwenyezi Mungu amuwafikishe kulitamka.
 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “Walakinieni watu wenu wanaokaribia kufa Laa ilaha illa llah   (Muslim)
 
Katika riwaya nyingine ya Ibn Hibaan amesema,“ Atakaye tamka maneno yake ya mwisho Laa ilaha illa llah ataingia peponi siku moja katika dahr hata likimpata litakalompata.”
 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema katika hadithi nyingine kuwa, “Atakayekufa na hali amekufa akifahamu kuwa hakuna Mola Apasae kuabudiwa kwa haki ila Allah basi mtu huyo ataingia peponi.” (Muslim)
 
Hali kadhalika katika hadithi yake nyingine amesema kuwa, “Atakayekufa na hakumshirikisha Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) na kitu chochote ataingia peponi.” (Muslim)
 
Katika Musnad ya Imam Ahmad imepokewa kuwa, “Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alimtembelea mgonjwa katika Ansaar akasema kumwambia yule mgonjwa, “Ee, mjomba sema, ‘Laa ilaha illa llah’ akasema (mpokeaji kuwa mtu huyu alikuwa ni mjomba au ami), “ni mjomba au baba mdogo” akasema, ‘bali ni mjomba’ akasema, “nikakhiyarishwa niseme, “Laa ilaha illa llah” Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akasema, “Naam.”
 
 
Katika hadithi nyingine sahihi iliyokuwa ni mashuhuri zaidi imepokewa kuwa, “Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alimwambia Ami yake Abi Talib alipokuwa katika sakaratul maut, “Ewe ami yangu sema, Laa ilaha illa llah, neno litakalo kufanya upate shufaa ya Allah (Subhaanahu wa Ta'ala).”
Share