16-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kumfunga macho na kumuombea atakapokufa

 
Kumfunga macho na kumuombea atakapokufa:
 
 
Imam Muslim amepokea, ‘Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) aliingia kwa Abu Salama macho yake yakiwa yamekodoka, akamfunga kisha akasema, “Hakika roho inapochukuliwa hufuatiwa na macho” akasikia kelele kutoka kwa watu wa Abu Salama, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akasema kuwaambia, “Msijiombee ila muombe dua njema, hakika malaika huitikia Amin kwa yale mnayoyaomba.” Kisha akasema tena, “Ee, Mwenyezi Mungu msamehe Abu Salama na nyanyua hadhi yake pamoja na waongofu, na uwaache baada yake pamoja na waliotangulia, utusamehe sisi na yeye Ee, Mola wa ulimwengu, lipanue kaburi lake na uliwekee nuru.”
Share