23-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kutangaza kifo kwa ajili ya maslaha

 

Kutangaza kifo kwa ajili ya maslaha:

 

 

Hakika kutangaza kifo cha Muislamu ni jambo lisilohimizwa kisheria, kutangazwa kifo cha Muislamu ni kwa haja kwa wale watakaomuosha, watakaomkafini, watakaomswalia na watakaomzika. Njia zinazoruhusiwa kisheria zitatumika kwa haja bila ya kuwepo kwa Taklifu yoyote kwa mfano: watu kujulishana huo msiba, au kwa njia ya simu kama ilivyo siku hizi, vile vile inajuzu kutumia vipaza sauti (microphone) kwa haja inayolazimu kama kutumika vijijini bila ya kuzidisha zaidi ya kutaja kifo chake na wakati wa kuswaliwa na mfano wa hayo.

Katika siku ambayo Mtume aliomboleza kifo cha Najashi siku aliyokufa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alikwenda katika mswala, akawapanga safu kisha akafanya takbir mara nne (Bukhari na Muslim)

Hali kadhalika alipoomboleza viongozi wa vita vya Mu’ta, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alisema, “Zaid alichukua bendera kisha akauawa baada ya hapo akachukuwa Jaafar nae akauawa kisha akachukuwa Abdullah bin Rawaaha naye akauawa…” (Bukhari)

Share