24-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kutangazwa kifo kwa lengo la kumuombea

Kutangazwa kifo kwa lengo la kumuombea:
 
Inajuzu kutangazwa kwa kifo cha Muislamu kwa lengo la kumuombea dua kutoka kwa wanawe, nduguze, jamaa na jirani zake. Katika Musnad ya Imam Ahmad kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alisema, “Je, nikujulisheni kuhusu jeshi lenu lenye kupambana? Lilikwenda likakutana na adui, Zaid akafa shahidi, wakamuombea kwa Mwenyezi Mungu na watu wakamuombea, kisha bendera ikashikwa na Jaafar bin Abi Talib nae akapigana na watu kwa ushujaa mkubwa akafa shahidi, nashuhudiwa shahada yake hiyo, wakamuombea, kisha bendera ikashikwa na Abdullah bin Rawaaha akapigana kwa ushujaa nae akafa shahidi, watu wakamuombea…”
Katika sahihi mbili: kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alipoomboleza kifo cha Najashi alisema, “Muombeeni msamaha ndugu yenu kwa Mola wenu.”
Share