27-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kuoshwa maiti upesi

 
Kuoshwa maiti upesi:
 
 
Katika mambo ya kheri ambayo humfikia maiti ni kufanya upesi katika kumtayarisha kwa kumkosha, kumkafini na kumzika.
 
Katika kuoshwa vinachungwa vifuatavyo:
 
· Idadi ya kuoshwa iwe ni mara tatu na zaidi ikibidi kwa haja kwa sharti kuwa idadi hiyo iwe ni witri: tatu, tano au saba na mfano wa haya.
 
· Itumike majani ya mkunazi au sabuni katika kila anapokoshwa ili kumsafisha vizuri zaidi.
 
· Muoshaji atumie sabuni au mfano wake kama vile siku hizi gloves inavyotumika na kuwepo na sitra yenye kumfunika maiti baada ya kuvuliwa nguo.
 
· Ni vizuri kutia kafuri katika maji haswa katika josho la mwisho au mafuta mazuri maadamu sio haramu, na inapokuwa ni haramu basi hayafai.
 
· Kucha za mwanamke zitapunguzwa na kuoshwa vizuri, hali kadhalika nywele zake kuchanwa na kufungwa vifundo vitatu nyuma yake.
 
·  Aanze kukosha sehemu za kulia kwanza na sehemu za udhu
 
·  Mwanamume hukosha wanaume, mwanamke hukosha wanawake, mume humuosha mkewe na mke humkosha mumewe.
 
·  Shahidi, aliyekufa katika vita hakoshwi.
Share