28-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kinachomlazimu mwenye kukosha

 
Kinachomlazimu mwenye kukosha:
·         Ni vizuri muoshaji awe ni mwenye kujua zaidi Sunna za josho na matendo yake katika jamaa na ndugu wa karibu zaidi wa maiti au mtu mwingine katika watu wenye elimu na fadhila.
·         Ni juu ya muoshaji kusitiri aibu za maiti, haifai kuhadithia anachokiona kwake, ama akiona kizuri kwa maiti basi na aseme hamna neno katika kuelezea ya kheri.
·         Ni juu ya mkoshaji katika tendo lake hili au amali yake hii njema ya kukosha anayofanya atarajie radhi za Allah (Subhaanahu wa Ta'ala)
Share