30-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Je, maiti itahamishwa kutoka katika nchi aliyofia na kupelekwa nchini kwake?

Je, maiti itahamishwa kutoka katika nchi aliyofia na kupelekwa nchini kwake?
 
Mtu anaweza kufa katika nchi isiyokuwa ile anayoishi au katika kijiji chake, kiasi cha kuwa wakati mwingine ikahitajika kumsafirisha kumrudisha katika nchi yake ya asili au ile anayoishi (ambapo ndipo penye watoto wake, ndugu na jamaa zake) je, jambo hilo linafaa kisheria?
Jibu: jambo hilo halifai kisheria kwani huchelewesha kuzikwa kwa maiti, kisha baada ya hapo ni kinyume na Sunna.
Imepokewa kutoka kwa Aisha (Radhiya Allaahu 'anhu) kuwa nduguye mmoja alikufa katika sehemu iitwayo Waadil Habasha akahamishwa kutoka sehemu ile, Aisha akawaambia waliomhamisha, ‘Linanihuzunisha (nyie kufanya hivyo) ni vizuri kama angezikwa sehemu ile aliyofia.’
Share