46-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Matamko yaliyokatazwa

Matamko yaliyokatazwa:
 
 Imezoeleka kwa baadhi ya watu kumwambia mfiwa aliyefiliwa na mtu wa karibu yake maneno haya, ‘Yaliyobaki yawe katika maisha yako’ haya ni matamko yasiyotakiwa kwani yaweza kufahamika maana yake kuwa, ‘kuwa maiti hakukamilisha umri wake, na kuwa kuna umri wake ambao hakuishi, hivyo basi huomba baki ya umri ambao hakuishi uende kwa jamaa na ndugu zake walio hai. Mwenyezi Mungu amebainisha kuwa ajal ya mtu itakapofika haicheleweshwi wala haiwahi saa wala dakika, kwa hivyo tena hakuna tena baki ya Umri wa yule aliyekufa.
 
Share