47-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Dua za Waislamu zinamnufaisha maiti

 

Dua za Waislamu zinamnufaisha maiti:

 

Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala) amesema, “Na waliokuja baada yao wanasema: Mola wetu Mlezi! Tughufurie sisi na ndugu zetu waliotutangulia katika Imani, wala usijaalie ndani ya nyoyo zetu undani kwa walio amini. Mola wetu Mlezi! Hakika Wewe ni Mpole na Mwenye kurehemu.” (59:10)

Katika hadithi yake Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “maombi ya Muislamu kwa nduguye ni yenye kujibiwa, katika kichwa chake kuna malaika aliyewakilishwa kila atakapomuombea nduguye kheri anasema malaika yule: Amin, nawe upate kama hivyo (ulivyomuombea nduguyo).” (Muslim)

Share