50-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kumtolea sadaka maiti

 

Kumtolea sadaka maiti:

 

Tunasoma katika sahihi mbili kuwa: mtu mmoja alisema, ‘Mama yangu alijisahau na lau angeliweza kusema angetoa sadaka, je, atapata ujira nikimtolea sadaka?’ Mtume akajibu, “Ndio atapata ujira na malipo kwa sadaka hiyo.” Hali kadhalika tunasoma katika sahihi ya Bukhari kuwa, “Sa’ad bin ‘Ubada alifiliwa na mama yake wakati hayupo, akasema, ‘Ee, Mtume wa Allah, mama yangu amefariki nami sipo, je, itamfaa lau nikimtolea sadaka? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akajibu, “Ndio (atanufaika kwa sadaka hiyo)” kisha Sa’ad akasema kama ni hivyo, ‘Basi nakushuhudia kuwa ukuta wenye mitende mingi ni sadaka yake.’

 

Share