54-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Au kijana mwema atakayemuombea dua

 
Au kijana mwema atakayemuombea dua:
 
Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala) amesema, “…Na useme: “Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama walivyonilea katika utoto.” (17:24)
Nae Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “atakapokufa mwanadamu matendo yake yote hukatika ila hubakia mambo matatu; sadaka yenye kuendelea, elimu yenye kunufaisha au kijana mwema atakayekuombea dua.” (Bukhari na Muslim)
Ama Abu Daud na Ibn Majah nao wamepokea kutoka kwa Abu Usaid Malik Ibn Rabia Assaidy amesema, ‘Tulipokuwa kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alitokea mtu mmoja wa kabila la Salama, mtu yule akamuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam), ‘Je, kuna kilichobakia katika wema ninaoweza kuwafanyia wazazi wangu baada ya kifo chao? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akajibu, “Ndio, kuwaombea dua na msamaha kwa Mwenyezi Mungu, kutekeleza ahadi ulizowapa baada ya kifo chao, kutembelea wagonjwa hali kadhalika kuwatembelea jamaa na ndugu ambayo haiwezikani bila ya wewe kuwa mtoto wao, na kuwakirimu rafiki zao.”
 
Share