56-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Je, huswali swala yake na ya babake au hufunga kwa funga yao?

Je, huswali swala yake na ya babake au hufunga kwa funga yao?
 
 
Amesema Imam Muslim katika utangulizi wa sahihi yake, ‘Amesema Muhammad kuwa, nimemsikia Abu Ishaka ibrahim bin Issa Attwalaqaan akisema, ‘Nilimuuliza Abdullah bin Mubaarak, ‘Ewe, Abu AbduRahman! Vipi kuhusu ile hadithi inayosema, “Hakika katika wema mzuri zaidi kufanya baada ya wema ni kuwaswalia wazazi wako pamoja na swala yako, na kuwafungia saumu pamoja na saumu yako.” Akasema kuwa, ‘Abdullah bin Muba’rak akasema, ‘Ewe, Abu Ishaka hadithi hii imetoka kwa nani? Akajibu, ‘Ni katika hadithi ya Shihaab bin Kharaash.’ Abdullah bin Muba’raka akasema, Huyu ni mtu anayeaminika’ Je, imetoka kwa nani?’ Nikasema, ‘Kutoka kwa al-Hajjaj bin Di’nar. Abdullah akasema, Huyu nae anaaminika’ Je, kutoka kwa nani? Nikasema, ‘kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam)’. akasema Abdullah bin Mubarak, ‘Ewe, Abu Ishaka hakika baina ya al-Hajjaj bin Di’nar na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) mafaawidh tanqatwih fiiha ahnaaq al-Matwy  lakini katika sadaka hakuna tofauti. Hapa Abdullah bin Mubaarak (rehema ya Allah iwe juu yake) anakusudiwa kuonesha kuwa hadithi yenyewe ni dhaifu lakini ile sehemu yenye kutaja sadaka ni sahihi hakuna tofauti miongoni mwa watu wenye elimu katika kujuzisha sadaka lakini si swala.
 
Share