58-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Je, ni ruhusa kwa wanawake kutembelea makaburi?

 
Je, ni ruhusa kwa wanawake kutembelea makaburi?
 
 

Wakati tunazungumzia suala hili yapasa kuangalia sura nyingi kama hizi zifuatazo:

Kwanza: Haifai kwa wanawake kusindikiza maiti na kuzika kwa mujibu wa maneno ya Ummu Atwiya (Radhiya Allaahu 'anhu), “Tumekatazwa kusindikiza jeneza walam yuuzam alayna. (Bukhari na Muslim)
Pili: inafaa kwa mwanamke kuzuru makaburi baada ya kuzika, ili kumuombea maiti, kwa sharti kuwa azingatie hukumu za kisheria kama vile kujisitiri vizuri, kuacha kupiga makelele katika bid’a na maasi. Katika hili wanawake na wanaume wanakuwa sawa sawa kulingana na kauli yake Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam), “Nilikuwa nimewakataza kwanza kuzuru makaburi lakini kuanzia sasa yatembeleeni.” (Muslim)
 
Tatu: kinachokatazwa kwa wanawake ni ziara za mara kwa mara makaburini, kwani ziara hizo za mara kwa mara hupoteza haki nyingi pamoja na udhaifu wa mwanamke katika mas’ala mazima ya misiba na kupiga mayowe na kujigaragaza kwa kuombeleza na mfano wa mambo kama hayo. Kama ilivyopokelewa katika hadithi nyingine inayosema, “Mwenyezi Mungu amewalaani wanawake wenye kwenda mara kwa mara makaburini.”
Share