59-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Matamko yanayotumika katika kuwaombea wafu makaburini

Matamko yanayotumika katika kuwaombea wafu makaburini:
 
Imepokewa katika sahihi Muslim kuwa, ‘Aisha (Radhiya Allaahu 'anhu) alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) Je, tunatakiwa tuseme nini kuwaombea waliokwisha zikwa makaburini?’ Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akamwambia, “ Sema, 
 
 
السَّلامُ عَلَـيْكُمْ أَهْلَ الدِّيارِ مِنَ المؤْمِنيـنَ وَالْمُسْلِمينَ، وَإِنّا إِنْ شاءَ اللهُ بِكُـمْ لاحِقُـونَ

( وَ يَرْحَمُ اللَّهُ الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنَّاوَالْمُسْتَأْخِرِينَ) نَسْـاَلُ اللهَ لَنَـا وَلَكُـمْ العَـافِيَةَ.                                             

Assalaam ala ahli diyaar minnal muuminina wal muslimina, wainna inshaAllah bikum llahiquuna.”          wayarhamu llaha al-Mustaqdimiina minna wal musta’khirina, Nas-alu Allaaha Lana wa lakum Al-'Aafiyah
 
“Amani ishuke juu yenu watu wa nyumba za waumini na waislamu, nasi apendapo Mwenyezi Mungu  tutakutana nanyi, tunamuomba Mwenyezi Mungu  atusamehe, sisi na nyinyi.  [Na Mwenyezi Mungu awarehemu wa mwanzo na wa mwisho] namuomba Mwenyezi Mungu  atupe sisi nanyi afya njema.
 
 Mtume anapokuwa kwake alikuwa akitoka usiku wa mwisho na akisema, “Assalamu alaykum dara Qawmi Muuminiin, Wa’atakum maa Tad’uuna Ghadan Muajala’n, Wainna InshaAllah bikum Laahiquun, Allahumma ghfir Liahli Baqiih Al-Gharqad.” (Muslim)
 
Share