18-Hadiyth Al-Qudsiy: Swawm Ni Yangu Na Ni Mimi Ndiye Ninayelipa

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 18

Swawm Ni Yangu Na Ni Mimi Ndiye Ninayelipa

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَال: ((يَقُولُ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: الصَّوْمُ لِي وَأَنَا أَجْزِي بِهِ، يَدَعُ شَهْوَتَهُ وَأَكْلَهُ وَشُرْبَهُ مِنْ أَجْلِي، وَالصَّوْمُ جُنَّةٌ وَلِلصَّائِمِ فَرْحَتَانِ، فَرْحَةٌ حِينَ يُفْطِرُ وَفَرْحَةٌ حِينَ يَلْقَى رَبَّهُ، وَلَخُلُوفُ فَمِ الصَّائِمِ أَطْيَبُ عِنْدَ اللَّهِ مِنْ رِيحِ الْمِسْكِ))  البخاري و مسلم و مالك والترمذي والنسائي وابن ماجه 

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye alisema: ((Allaah Aliyetukuka na Jalali Anasema: Swawm ni Yangu na ni Mimi ndiye ninayelipa. (Mtu) huacha matamanio yake, chakula chake, kinywaji chake kwa ajili Yangu. Swawm ni ngao, na yule anayefunga ana furaha mbili; Furaha anapofuturu na furaha anapokutana na Mola wake. Mbadiliko wa harufu ya pumzi zake (kutoka mdomoni) ni bora kwa Allaah kuliko harufu ya misk)) [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik, At-Tirmdihiy, An-Nasaaiy na Ibn Maajah]

 

Share