32-Hadiyth Al-Qudsiy: Mtu Anayejiua Anaharamishwa Jannah (Haingii Peponi)

Hadiyth Al-Qudisy

Hadiyth ya 32

Mtu Anayejiua Anaharamishwa Jannah (Haingii Peponi)

 

عَنْ جُنْدَبُ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((كَانَ فِيمَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ رَجُلٌ بِهِ جُرْحٌ، فَجَزِعَ فَأَخَذَ سِكِّينًا فَحَزَّ بِهَا يَدَهُ، فَمَا رَقَأَ الدَّمُ حَتَّى مَاتَ، قَالَ اللَّهُ تَعَالَى: بَادَرَنِي عَبْدِي بِنَفْسِهِ حَرَّمْتُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ)) البخاري

Kutoka kwa Jundub bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Alikuweko miongoni wa wale waliokutangulieni mtu ambaye alijeruhiwa. Alikuwa na maumivu makubwa kwa hivyo alichukua kisu akajikata mkononi mwake, damu haikusita kutoka mpaka akafa. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akasema: Mja wangu kaniwahi kwa (kuitoa) nafsi yake; nimemuharamishia yeye Jannah)) [Al-Bukhaariy]

 

Share