33-Hadiyth Al-Qudsiy: Mwenye Kusubiri Anapoondokewa Na kipenzi Chake Hulipwa Jannah

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 33

 Mwenye Kusubiri Anapoondokewa Na kipenzi Chake Hulipwa Jannah

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَقُولُ اللَّهُ تَعَالَى مَا لِعَبْدِي الْمُؤْمِنِ عِنْدِي جَزَاءٌ إِذَا قَبَضْتُ صَفِيَّهُ مِنْ أَهْلِ الدُّنْيَا ثُمَّ احْتَسَبَهُ إِلَّا الْجَنَّةُ)) البخاري

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Ta’aalaa Anasema: Haitokuwa jazaa ya mja wangu Muumini Ninapomchukulia kipenzi chake bora katika ahli wa duniani kisha akastahamili kwa ajili Yangu, haitakua ila ni (kumuingiza) Jannah)) [Al-Bukhaariy]

Share