42-Hadiyth Al-Qudsiy: Watu Wa Jannah Watapata Ridhaa Ya Allaah

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 42 

Watu Wa Jannah Watapata Ridhaa Ya Allaah

 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ اللَّهَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى يَقُولُ لِأَهْلِ الْجَنَّةِ: يَا أَهْلَ الْجَنَّةِ!  فَيَقُولُونَ لَبَّيْكَ رَبَّنَا وَسَعْدَيْكَ،   فَيَقُولُ: هَلْ رَضِيتُمْ؟  فَيَقُولُونَ وَمَا لَنَا لَا نَرْضَى وَقَدْ أَعْطَيْتَنَا مَا لَمْ تُعْطِ أَحَدًا مِنْ خَلْقِكَ،   فَيَقُولُ:  أَنَا أُعْطِيكُمْ أَفْضَلَ مِنْ ذَلِكَ،   قَالُوا: يَا رَبِّ وَأَيُّ شَيْءٍ أَفْضَلُ مِنْ ذَلِكَ؟  فَيَقُولُ: أُحِلُّ عَلَيْكُمْ رِضْوَانِي فَلَا أَسْخَطُ عَلَيْكُمْ بَعْدَهُ أَبَدًا)) البخاري،  مسلم و الترمذي

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Tabaaraka wa Ta’aalaa Atawaambia watu wa Jannah: Enyi watu wa Jannah! Watasema: Labeka Rabb wetu tuko chini ya amri Yako na kheri zote zimo katika Mikono Yako. Kisha Atasema: Je, mmeridhika?  Watasema: Vipi tusiridhike na hali Umetupa ambayo Hukumpa yeyote mwengine katika viumbe Vyako? Kisha Atasema:  Nitakupeni kilichobora kuliko hayo. Watasema: Ee Rabb, ni kipi kilicho bora kuliko haya? Atasema: Nitafanya ridhaa (mapenzi) Yangu iwateremkie na baada ya hapo Sitoghadhibika nanyi tena abadan)) [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhy]

 

Share