013-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Du'aa Za Kufungulia Swalah

 

 

DU'AA ZA KUFUNGULIA

 

Kisha alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akianza kusoma kwake kwa aina nyingi za du'aa ambazo akimsifu na kumtukuza na kumuadhimisha Allaah (سبحانه وتعالى). Alimuamrisha "mtu aliyeswali vibaya" afanye hivyo akimwambia: ((Swalah ya mtu haikamiliki hadi atamke Takbiyr, amsifu Allaah (سبحانه وتعالى), amtukuze na amuadhimishe asome iliyo nyepesi katika Qur-aan…..))[1] .

 

Alikuwa akisoma du'aa zozote katika hizi zifuatazo:

 

 1.

 

 

 

"Ee Allaah! Niweke mbali na madhambi yangu kama Ulivyoweka mbali baina ya Mashariki na Magharibi, Ee Allaah! Nitakase na madhambi yangu kama vile inavyotakaswa nguo nyeupe na uchafu, Ee Allaah!  Nisafishe na madhambi yangu kwa theluji na kwa maji na kwa barafu"[2]

(Na alikuwa akisema katika swala za fardhi):

2.

 

 

 

“Nimeuelekeza uso wangu kwa yule Ambaye Ameumba mbingu na ardhi hali ya kumtakasia yeye dini yangu, na sikuwa mimi ni katika washirikina, hakika Swalah yangu na kuchinja  kwangu na uhai wangu, na kufa kwangu ni kwa Allaah Bwana wa viumbe vyote, Hana mshirika, na kwa hilo nimeamrishwa, nami na mimi ni wa kwanza waliojisalimisha.[3]  Ee Allaah! Wewe ndiye Mfalme, hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, Wewe ndiye Bwana wangu na mimi ni mtumwa (mja) Wako[4] Nimedhulumu nafsi yangu, na nimekiri madhambi yangu kwa hivyo nisamehe madhambi yangu yote, hakika hasamehe madhambi, ila Wewe. Na niongoze kwenye tabia nzuri, kwani haongozi kwenye tabia nzuri ila Wewe. Na Niepushe na tabia mbaya, kwani hakuna wa kuniepusha na tabia mbaya ila Wewe. Naitikia mwito Wako, na nina furaha kukutumikia.[5] Kheri zote ziko mikononi Mwako, na shari haitoki Kwako[6], Na ameongoka yule Uliyemuongoa, mimi nimepatikana kwa ajili Yako, hapana penye uokovu wala wa pa kukimbilia isipokuwa Kwako, umetakasika, na umetukuka, nakutaka msamaha na ninarejea Kwako (kwa kutubia).”

 

Alikuwa akisema hivyo katika Swalah za fardhi na za Sunnah[7]

 

 

 

3. Hii du’aa ni kama iliyo juu bila ya:

 

 

 

 

“Wewe Ni Mola wangu nami ni mja Wako…”

 

Hadi mwishoni pamoja na nyongeza ifuatayo:

 

 

 

 

 

“Ee Allaah, Wewe Ni Mfalme, hapana apasaye kuabudiwa isipokuwa Wewe, Kutakasika ni Kwako na Sifa njema zote ni Zako”[8]

 

 

4- Kama na Namba 2 hadi,

 

 

 

 

 

“…nami ni Muislamu wa mwanzo,

 

Na akiongeza,

 

 

 

 

 

 

Ewe Allaah, niongoze kwenye tabia njema (nzuri) na vitendo vyema haongozi kwenye uzuri wake ila Wewe. Niepushe na tabia mbaya na vitendo vibaya hakuna mwenye uwezo wa kupesuha??? ubaya wake ila Wewe [9].

 

 

5-

 

 

 

 

 

Kutakasika ni Kwako[10] Ee Allaah, na sifa njema zote ni Zako[11], na limetukuka Jina Lako[12], na Utukufu ni Wako[13], na hapana apasae kuabudiwa kwa haki, asiyekuwa Wewe[14]

Alisema (صلى الله عليه وآله وسلم) pia: ((Hakika maneno yanayopendwa kabisa na Allaah ni mja Wake anaposema: (سبحانك اللهم) Umetukuka Ewe Allaah…”[15]

 

 

6- Kama ilivyo juu kwa kuongeza katika Swalah za usiku:

 

 

 

                                                               

 

 

“Hapana apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah”

 

Mara tatu na

 

 

 

 

“Allaah ni Mkubwa”

 

 

Mara tatu

 

 

7-

 

 

 

 

 

“Allaah Ni Mkubwa, Na sifa njema ni za Allaah kwa wingi, Ametakasika Allaah asubuhi na jioni.”

 

 

 

 

 

Mmoja wa Maswahaba alifungua Swalah yake kwa du’aa hiyo, Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) alisema: ((Imenipendeza hiyo (du'aa) kwani kwayo milango ya Pepo imefunguliwa))[16]

 

 

8- 

 

 

 

 

 

“Sifa njema ni za Allaah, sifa nyingi, nzuri, zenye Baraka”

 

Mtu mwengine alifungua Swalah yake kwa du’aa hiyo, kisha Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Nimewaona Malaika kumi na mbili wakishindana nani atakayeipeleka juu))[17]

 

 

9-

 

 

“Ee Allaah ni Zako sifa njema, Wewe ndiye nuru[18] ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na ni Zako sifa njema. Wewe ndiye Mwenye kuzisimamia[19] mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, [na ni Zako sifa njema, Wewe ni Mfalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake],  na sifa njema ni Zako, Wewe ni Haqq, na ahadi Yako ni ya Haqq, na neno Lako ni Haqq, na kukutana Nawe ni Haqq, na Pepo ni Haqq, na Moto ni Haqq, na Sa’ah (Qiyaamah) ni Haqq, na Mitume ni Haqq, na Muhammad ni Haqq, Ee Mola Kwako nimeweka imani yangu, na Kwako nimetegemea, na Kwako ndio nakurejelea, nimepigana kwa ajili Yako, na kwa hukumu Zako ndio nazifuata zinihukumu, [Wewe ndiye Mola wetu na Kwako ndio tunaishia, nisamehe niliyoyatanguliza na niliyoyachelewesha, na niliyoyaficha  na niliyoyatangaza], [Na yote unayoyajua kutoka kwangu] Wewe ndiye mwenye kutanguliza na ndiye mwenye kuchelewesha, [Wewe ni Mola wangu] hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe[20]; 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema hivi katika Swalah ya usiku alipokuwa akisoma du'aa ifuatayo[21]:

 

10-

 

 

 

 

“Ewe Mwenyezi Mungu  Mola wa Jibiriyl na Mikaaiyl na Israafiyl, Muumba wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa mambo yaliojificha na yaliyowazi, Wewe unahukumu baina ya waja Wako katika mambo ambayo walikuwa wakitofautiana, niongoze mimi kwenye  haki katika yale waliyotafautiana kwa ruhusa Yako.  Hakika Wewe unamuongoza umtakae kwenye njia iliyonyoka[22]

 

 

11- Alikuwa akisema Takbiyr, Tahmiyd, Tasbiyh, Tahliyl na Istighfaar mara kumi kila moja na akisema:

 

 

 

 

 

“Ee Allaah, nighufurie na niongoze na niruzuku [Na Nisamehe madhambi yangu]” mara kumi kisha akisema:

 

 

 

 

 

“Ee Allaah, Najikinga Kwako na dhiki za Siku ya Hisabu”[23]

 

Mara kumi

 

 

 

12-

 

 

 

 

“Allaah ni Mkubwa [mara tatu] Mwenye Ufalme, Nguvu, Ufakhari na Utukufu”[24]

 

 





[1] Al-Bukhaariy, Muslim na Ibn Abi Shaybah (12/110/2) imetolewa katika Al-Irwaa (Namba 8)

[2] Abu Daawuud na Al-Haakim ambaye amekiri kuwa ni Swahiyh na Adh-Dhahabiy amekubaliana.

 

[3]  Imesimuliwa katika usimulizi mwingi, katika mwengine, 'Wa Anaa Minal-Muslimiyn’ (Mimi ni miongoni wa Waislamu). Inaweza kuwa ni kutokana na makosa ya usimulizi mmojawapo, na ushahidi mwingine unaelekeza hapo, kwa hiyo mwenye kuswali aseme: ‘Wa Anaa Awwalul-Muslimiyn’ (Nami ni Muislamu wa mwanzo). Hakuna makosa hivyo, kinyume na watu wanavyosema kwa uoni kwamba inamaanisha "Mimi ni Muislamu wa kwanza mwenye sifa hii, na watu wengine hawana sifa hii". Lakini sio hivyo, ibara hii inaashiria kushindana katika kutekeleza amri. Hii ni sawa na ((Sema: Ingelikuwa ar-Rahmaan ana mwana, basi mimi ningelikuwa wa kwanza kumuabudu)) [Az-Zukhruf, 43: 81] na kauli ya Muusa ('Alayhis-Salaam) ((na mimi ni wa kwanza wa Waumini)) [Al-A'raaf 7: 143].

[4]  Al-Azhariy amesema kwamba, "Siabudu chochote kingine isipokuwa Wewe"

[5]  Labbayk: Niko thabiti na daima niko katika utiifu Wako. Sa'dayk: Furaha kubwa kuwa katika amri Yako na kufuata kwa dhati dini Uliyoichagua.

[6]  Yaani, Uovu haunasibishwi kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kwa sababu hakuna chochote kibaya katika vitendo Vyake, kwani vyote ni vyema vikianzia kutoka uadilifu, fadhila na hikma vyote ambayo ni kheri na havina shari ndani yake bila ya kuwa na shari ndani yake. Kwa sababu shari imekuwa shari kwa sababu hauwezi kurudia kwa Allaah. Ibn Al-Qayyim (Rahimahu-Allaah) amesema: "Yeye ni Muumba wa mema na maovu, lakini maovu yako katika baadhi ya viumbe Vyake, na sio katika kuumba Kwake na sio katika vitendo Vyake. Kwa ajili hiyo Ametakasika na dhulma ambayo asili yake ni kuweka kitu katika sehemu nyingine isiyopasa. Haweki kitu isipokuwa katika mahali panapostahiki ili yote yawe mema. Lakini uovu ni kuweka kitu mahali pasipostahiki. Kinapowekwa katika mahali panapostahiki, huwa si kiovu, kwa hiyo jua kuwa uovu hautoki Kwake.  Lakini ikisemwa: Kwa nini Ameumba maovu? Nitasema: Ameumba, na vitendo Vyake ni vizuri sio viovu kwani kuumba na vitendo vinasimama na Allaah, haiwezekani uovu kufanywa au kuhusishwa na Allaah. Chochote kilichokuwa kiovu hakiwezi kurudishwa kwa Allaah, ama vitendo na Alivyoviumba vinaweza kuhusishwa Naye, na vinakuwa ni vyema". Majadiliano muhimu yaliyobakia na kimalizio chake kitapatikana katika kitabu chake Shifaa Al-'Aliyl fiy Massail al-Qadhwaa wal-Qadar wat-Ta'liyl – taz (uk. 178-206).

[7] Muslim, Abu 'Awaanah, Abu Daawuud, An-Nasaaiy, Ibn Hibbaan, Ahmad, Ash-Shaafi'iy na At-Twabaraaniy. Walioeleza kuwa ni Swalah za Sunnah wamekosea.

[8]  An-Nasaaiy ikiwa na isnaad Swahiyh.

[9]  An-Nassaiy na Ad-Daaraqutwniy ikiwa na isnaad Swahiyh.

[10]  Nakutukuza ina maana kwamba nazingatia kuwa Umetakasika na kasoro yoyote. Na ‘Sifa njema’ maana yake ni kuwa tumezijua vizuri sifa Zako. Na ‘Kutakasika’ maana yake ni wingi wa kutakasika kwa jina Lako, kwa sababu kila la kheri linapatikana katika kulitaja jina Lako. ‘limetukuka Jina Lako’ maana yake ni kuwa limenyanyuka juu jina Lako (utukufu wako).

[11]  Tumeshikamana katika kukusifu.   

[12]  Baraka za Jina Lako ni kubwa, kwani makubwa yaliyo mazuri hutokana na kukumbuka Jina Lako.

[13]  Utukufu na Nguvu Zako.

[14]  Abu Daawuud na Al-Haakim ambaye amekiri ni Swahiyh na Adh-Dhahabiy amekubaliana. 'Uqayl amesema (Uk. 103) "Hii imesimuliwa kupitia njia mbalimbali kwa isnaad Swahiyh". Imetolewa katika Al-Irwaa (Namba 341) Imesimuliwa na Ibn Mandah katika At-Tawhiyd (123/2) kwa isnaad Swahiyh na An-Nasaaiy katika Al-Yawm wal-Laylah ikiwa ni mawquuf na marfuu'  kama katika Jaami' Al-Masaaniyd ya Ibn Kathiyr (Mj. 3 Kifungu 2. Uk. 235/2)

 

[15] Abu Daawuud na Atw-Twahaawiy kwa isnaad Swahiyh.

[16] Muslim Na Abu Awaanah; At-Tirmidhiy kasema ni Swahiyh. Kadhalika Abu Na’iym ameisimulia katika ‘Akhbaar Aswbahaan’ (1/210) kutoka kwa Jubayr bin Mutw-am ambaye alimsikia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) akiisoma kwenye Swalah ya Sunnah.

[17] Muslim na Abu 'Awaanah

[18] Wewe Ndiye Mwenye kuzipa mwanga na Kwayo ndio Wanaopata uongofu kutoka Kwako.

[19] Mwenye kuhifadhi na Mchungaji wao.

[20]  Al-Bukhaariy na Muslim, Abu 'Awaanah, Abu Daawuud, Ibn Nasr na Ad-Daarimiy.

[21]  Ingawa inapaswa kusomwa katika Swalah za fardhi pia, isipokuwa kwa Imaam kwa khofu ya kurefusha Swalah kwa Maamuma.

[22] Muslim na Abu 'Awaanah.

[23]   Ahmad, Ibn Abi Shaybah (12/119/2), Abu Daawuud na At-Twabaraaniy katika Mu'jam al-Awswatw (62/2) ikiwa na isnaad moja Swahiyh na nyingine Hasan.

[24]   At-Twayaalisiy na Abu Daawuud ikiwa na isnaad Swahiyh.

Share