014-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kisomo Katika Swalah, Na Kusoma Aayah Moja Moja

 

KISOMO (TILAAWAH)

 

Kisha alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akijikinga kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kusema:

 

A’udhu bil Llaahi minash Shaytwaanir Rajiiymi Min Hamzihii Wa Nafkhihii Wa Nafathihi

“Najilindia na Allaah kutokana na Shaytwaan aliyefukuzwa, najilinda na (kutokana na) wazimu wake[1] na kiburi chake, na ushairi [kutabana] wake[2]

Mara nyingine huongeza kwa kusema,

A’udhu bil Llaahis Samiy’il ‘Aliymi Minash Shaytwaanir…

Najikinga kwa Allaah, Mwingi wa Kusikia, Mwenye Ujuzi, kutokana na Shaytwan…[3]

Kisha husoma,

Bismi-Llaahir Rahmaanir Rahiym

Kwa Jina la Allaah,Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.

Hakuwa akinyanyua au kupaza sauti[4]

 

 

 

KUSOMA AAYAH MOJA MOJA

 

Kisha alikuwa Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma Suratul-Faatihah na akigawanya (kisomo chake,) kwa kuisoma Aayah moja moja; kama hivi:

 

 

BismiLlaahir Rahmaanir Rahiym

[Kisha hupumua/husimama, kisha husema:]

AlhamduliLlaahi Rabbil ‘Aalamiyn

[Kisha hupumua/husimama, kisha husema:]

Ar-Rahmaanir-Rahiym

[Kisha hupumua/husimama, kisha husema:]

Maaliki Yawmid Diyn

Kisomo chake kilikuwa kama hivyo, hadi mwisho wa Surah. Na hivyo hasa ndivyo ilivyokuwa kisomo chake chote, kila anaposoma huwa anasimama/anapumua mwisho wa Aayah na wala haiunganishi na Aayah inayofuatia[5].

mara nyingine alikuwa akiisoma bila ya kuivuta/bila ya kutia madda[6] (alisoma):

Malik Yawmid Diyn

Mfalme wa Siku Ya Qiyaamah

 

(badala ya

Maaliki Yawmid Diyn

 

Mwenye kumiliki Siku Ya Qiyaamah)

 

 

 





[1]  Maneno matatu ya Kiarabu; hamz, nafkh na nafth yamefasiriwa na baadhi ya wapokezi kuwa hamz ni aina ya wazimu, na nafkh ni kiburi, na nafth ni ushairi; yametafsiriwa hivyo hivyo na msimulizi; tafsiyr zote tatu zimepokewa (zimerudiwa pia) marfuu’an kwa Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa isnaad Swahiyh Mursal (Ni hadiyth katika isnaad yake hakutaja Swahaba, bali kataja Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم)). Na kusudio la (kwa) 'ushairi' [kutabana] hapa ni mashairi yasiyokubalika/yasiyo na heshima/yenye kudharauliwa (ina maana kwa majaribio yasiyo na mafanikio) kwani Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika katika baadhi ya ushairi kuna (ni) hikma)) [Al-Bukhaariy)

[2] Abu Daawuud Ibn Maajah, Ad-Daaraqutwny na Al-Haakim ambaye pamoja na Ibn Hibban na Adh-Dhahaabiy wamesema ni Swahiyh. Imetolewa pamoja  na inayofuatia katika Al-Irwaa Al-Ghaliyl (342)

 

[3]   Abu Daawuud na At-Tirmidhiy kwa isnaad nzuri. Ahmad ameinukuu katika Massail ya Ibn Haaniy 1/50

[4]   Al-Bukhaariy, Muslim, Abu 'Awaanah, At-Twahaawiy na Ahmad.

 

[5]Abu Daawuud na Sahmiy (64-65); Al-Haakim amesema kuwa ni Swahiyh na Adh-Dhahabiy amakubaliana naye. Imetolewa katika Al-Irwaa (343). Na ameipokea Abu 'Amr Ad-Daaniy katika Al-Muktafaa (5/2) na kasema: Hadiyth hii ina njia nyingi na ndiyo tegemeo katika mlango huu, kisha akasema: (na) Kundi la Maimamu wengi waliotangulia na Maqurraa (wasomaji wa Qur-aan) waliopita walikuwa wakipendelea kusimama katika kila Aayah hata kama (Aayah nyingine) itakuwa imefungamana  katika maana na Aayah ijayo") Nasema: Sunnah hii imepuuzwa na Maqurraa (wasomaji wa Qur-aan) wengi wa nyakati hizi, achilia mbali wengineo ambao si Maqurraa.

[6] Tamaam Ar-Raaziy katika Al-Fawaaid, Ibn Abu Daawuud katika Maswaahif (7/2), Abu Nu'aym katika Akhbaar Aswbahaan (1/104) na Al-Haakim ambaye amesema kuwa ni Swahiyh na Adh-Dhahaby amekuliana naye, qiraa/kisomo hichi  ‘Malik’ ni mutawaatir pia kama kilivyo kile qiraa cha kwanza ‘Maalik’.

Share