023-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Alivyokuwa Akisoma (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Swalah Mbalimbali. 1 - Swalah Ya Adhuhuri

 

1-   SWALAH YA ADHUHURI

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma katika Rakaa mbili za mwanzo Suratul-Faatihah na Surah mbili, hurefusha ya kwanza kuliko ya pili.([1])

 

Mara nyingine alikuwa akiirefusha urefu ambao ilikuwa inaweza kufika kuqimiwa kwa Swalah ya Adhuhuri, na aliweza mtu kwenda Al-Baqiy' kukidhi haja yake, [kisha aende nyumbani kwake], kutawadha, kisha aje hali ya kuwa Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiwa bado yuko katika Rakaa ya mwanzo, kwa namna alivyokuwa akiirefusha([2]).

 

(Pia) walikuwa wakidhania kwamba alikuwa akifanya hivyo ili watu waweze kuidiriki Rakaa ya mwanzo.([3])

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma katika kila Rakaa ya hizo Rakaa mbili, kadiri ya Aayah thelathini, kiasi cha kusoma As-Sajdah [32-30] na ikiwemo al-Faatihah.([4]) (na kufuatia As-Sajdah [32-30])

 

Mara nyingine alikuwa akisoma:

((وَالسَّمَاء وَالطَّارِقِ))

 

((Naapa kwa mbingu na kinachokuja usiku!)) [At-Twaariq: 86-17], na

 

 

((وَالسَّمَاء ذَاتِ الْبُرُوجِ))

 

((Naapa kwa mbingu yenye Buruji!)) [Al-Buruuj: 85-22], na

 

((وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَى))

 

((Naapa kwa usiku unapo funika!)) [Al-Layl: 92-21], na mfano wa Surah zilizofanana na hizi.([5])

 

Na huenda akasoma

 ((إِذَا السَّمَاء انشَقَّتْ))

 

((Itapochanika mbingu)) [Al-Inshiqaaq: 84-25], na mfano wake.([6])

 

Walikuwa wakiweza kuelewa kwamba alikuwa anasoma katika Adhuhuri na Alasiri kutokana na mtikisiko wa ndevu zake.([7])

 

 

 

[1]   Al-Bukhaariy na Muslim.

[2]   Muslim na Al-Bukhaariy katika Juz-u Al-Qiraat (Makala ya Tilaawah).

[3]   Abu Daawuud ikiwa na isnaad Swahiyh na Ibn Khuzaymah (1/165/1).

[4]   Ahmad na Muslim.

[5]  Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na Ibn Khuzaymah (1/67/2). Wawili wa mwisho wamesema kuwa ni Swahiyh.

[6]   Ibn Khuzaymah katika Swahiyh yake (1/67/2).

[7]   Al-Bukhaariy na Abu Daawuud.

Share