024-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kisomo Chake (صلى الله عليه وآله وسلم) Cha Aayaat Baada Ya Al-Faatihah Katika Rakaa Mbili Za Mwisho

KISOMO CHAKE (صلى الله عليه وآله وسلم) CHA AAYAAT BAADA YA AL-FAATIHAH KATIKA RAKAA MBILI ZA MWISHO

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akizifanya Rakaa mbili za mwisho fupi zaidi kulinganisha na Rakaa mbili za mwanzo kiasi cha nusu yake, kiasi cha Aayah kumi na tano,([1]) na pengine alifupisha katika Rakaa mbili za mwisho kwa kusoma al-Faatihah pekee.([2])

 

Alikuwa mara nyingine akiwasikilizisha Aayah.([3]) Na walikuwa wakisikia kutoka kwake mvumo wa kisomo chake:

 

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى

 

((Litakase jina la Mola Aliye juu kabisa)) [Al-A'laa 87-19],

na

 

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

 

((Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?)) [Al-Ghaashiyah 88-26].([4])

 

 

Mara nyingine husoma:

 

((وَالسَّمَاء ذَاتِ الْبُرُوجِ))

 

((Naapa kwa mbingu yenye Buruji!)) [Al-Buruuj 85-22], na

 

((وَالسَّمَاء وَالطَّارِقِ))

 

((Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!)) [Atw-Twaariq 86-17], na Sura nyinginezo mfano wa hizi mbili.([5])

 

Mara nyingine alikuwa akisoma:

 

((وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَى))

 

((Naapa kwa usiku unapofunika!)) [Al-Layl 92-21], Na mfano wake.([6])

 

 

[1] Ahmad na Muslim. Katika Hadiyth hii, kuna dalili kwamba kusoma Surah zaidi ya Suratul-Faatihah katika Rakaa mbili za mwisho ni Sunnah, na Maswahaba wengi walifanya hivyo. Miongoni mwao ni Abu Bakr (رضي الله عنه). (Pia) na ni rai ya Imaam Ash-Shaafi'iy, na ni sawa tu kama itakuwa katika Adhuhuri au katika Swalah nyinginezo. Maulamaa waliofuatia, Abul-Hasanaat Al-Laknawiy katika ((At-Ta’aliyq Al-Mummajad ‘Alaa Muwattwa Muhammad)) (Uk. 102) (akasema:"Na baadhi ya wafuasi wetu wamekuja na rai ya ajabu, kwani waliwajibisha Sajdatus-Sahw (Sajda ya kusahau) kwa kusoma Surah katika Rakaa mbili za mwisho. Na kwa hakika wamejibiwa na wenye kutoa maelezo/ sharh ya Al-Maniyyah; Ibraahiym Al-Halabiy na Ibn Amiyr Haaj na wengineo, wamejibiwa majawabu mazuri mno. Bila shaka wale waliosema hivyo haikuwafikia Hadiyth iliyotaja hayo, na lau kama imewafikia wasingelisema hivyo"

[2] Al-Bukhaariy Na Muslim.

[3] Ibn Khuzaymah katika Swahiyh yake (1.67/2) na Adh-Dhiyaa Al-Maqdsiy katika Al-Mukhtaarah ikiwa na isnaad Swahiyh.

[4] Al-Bukhaariy katika Makala ya Tilaawah, na At-Tirmidhiy ambaye amekiri kuwa ni Swahiyh.

[5]   Muslim na At-Twayaalisiy.

[6]   Al-Bukhaariy na Muslim.

Share