01-Matendo Mema Na Athari Yake Katika Utajiri Na Ukunjufu Wa Rizki: Utangulizi

 

Utangulizi

 

Shukrani zote zinamstahiki Allaah, tunamtukuza na tunamtegemea, tunaomba msamaha kwake, tunataka kinga kwa Allaah kutokana na shari ya nafsi zetu na matendo maovu yetu aliyeongozwa na Allaah hakuna wa kumpoteza na aliyepotea hakuna wa kumuongoza. Tunashuhudia hakuna mola wa kuabudiwa kwa haki ila Allaah Pekee na tunashuhudia kwamba Muhammad ni Mja Wake na Mtume Wake.

 

Ama baada, ametaja Allaah rizki ya viumbe katika Qur-aan Tukufu sehemu nyingi, na hii ni dalili ya ukubwa wa Allaah Aliyetukuka na nguvu Zake, kwani Ameumba viumbe na Akatawalia rizki zao, pia ni dalili juu ya rehma  kwa waja Wake na ukarimu Wake mkubwa, Naye ni Tajiri hahitaji kitu kwa viumbe, Naye ni Mtoaji kwa wote.

 

Amesema Allaah:

 

“Sikuwaumba majini na watu illa wapate kuniabudu, Sitaki kwao rizki wala Sitaki wanilishe, kwa yakini Allaah Ndiye Mtoaji wa riziki, Mwenye nguvu, madhubuti.” Adh-Dhariyaat: 57

 

Na Amejaalia AllaahAllaah matendo mema yanaendana na imani na ni sharti ya kupata maisha mazuri na malipo mazuri zaidi Akhera, Amesema Allaah :

 

“Mwenye kutenda mema katika mwanaume au mwanamke naye ni Muumin, Tutamuhuisha maisha mema na Tutawalipa ujira wao kwa mema waliyokuwa wakiyatenda.”

 

Hakika maisha yamewahadaa watu wakatopea nafsi zao katika mali, wakawa wanakimbizana kutafuta rizki kwa njia yoyote iwe halali au haramu, wakafuata nafsi zao  maisha yao yakawa dhalili, wakasahau kitabu cha Allaah na Sunnah, ambavyo ndani yake kuna ponyo (tatuzi) na kila kheri, navyo ni njia ya maisha mazuri na rizki pana na kheri nyingi katika dunia na Akhera.

 

Na sababu ya riziki na baraka ni matendo mema.

 

 

Share