02-Matendo Mema Na Athari Yake Katika Utajiri Na Ukunjufu Wa Rizki: Rizki Ni Makadirio Kutoka Kwa Allaah

 

A.    Rizki Ni Makadirio Kutoka Kwa Allaah

 

Allaahu Ameandika riziki za viumbe kabla hajawaumba, kwani elimu ya Allaah imezunguka kila kitu, hakuna kinachotembea ardhini ila imeandikwa riziki yake na ajali yake na vyote vinavyohusiana naye katika dunia na akhera.

 

 Amesema Allaah :

 

“Na hakuna mnyama yeyote (yaani kiumbe chochote) katika ardhi ila riziki yake iko juu kwa mwenyezi Mungu, na Anajua makao yake ya milele na mahali pake pa kupata tu. (napo ni hapa duniani) Yote yamo katika Kitabu kinachodhihirisha (kila kitu).” Huud: 6

 

 Ametupa habari Allaah Yeye ndiye mwenye kusimamia riziki ya viumbe vyote mdogo wao na mkubwa wao wa baharini na nchi kavu.

 

 “na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyoahidiwa.” Adh-Dhaariyaat: 22 

 

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uud amesema, amesema Mtume:

 

“Hakika mmoja mwenu anakusanywa katika tumbo la mama yake siku arobaini kisha inakuwa pande la damu mfano wa hivyo (siku 40) kisha inakuwa pande la nyama mfano wa hivyo, kisha Allaah Anamtumia Malaika kwa maneno manne, anamwandikia matendo yake, ajali yake, rizki yake, ni muovu au mwema, kisha anampulizia roho. Na mtu atatenda matendo ya watu wa motoni mpaka inakuwa baina yake na kuingia motoni usawa wa dhiraa inamtangulia Kitabu, anatenda matendo ya watu wa peponi na anaingia peponi.

Na kuna mtu anatenda matendo ya watu wa peponi mpaka inakuwa baina yake na kuingia usawa wa dhiraa, inamtangulia Kitabu anatenda matendo ya watu wa motoni akaingia motoni…” Al-Bukhaariy

 

Na kutoka kwa Anas Bin Maalik Amesema, Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam):

 

“Hakika Allaah Amemuwakilisha katika tumbo la uzazi Malaika anasema, Ee Mola tone la manii, Ee Mola pande la damu, Ee mola pande la nyama, atapotaka kuliumba anasema ewe Mola ni mwanaume au mwanamke? muovu au mwema? na ipi rizki yake? na ni ipi ajali yake? Anamwandikia hilo katika tumbo la mama yake.” Al-Bukhaariy

 

Share