030-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kisomo Chake (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Swalah Ya Janaazah

 

10- SWALAH YA JANAAZAH

 

"Sunnah ni kusoma Suratul Faatihah[1] [na sura nyingineyo][2]. Pia "Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akikaa  kimya kwa muda baada ya Takbiyr ya kwanza"[3]

 

 

KUSOMA KISOMO VILIVYO NA KUITENGENEZA SAUTI UNAPOSOMA

 

Alikuwa   (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma - kama Alivyoamrishwa na Allaah - Qur-aan vilivyo – kama inavyotakiwa kusomwa, mtu anatakiwa achunge hukumu za kuisoma-, bila ya kwenda mbio wala kuharakiza, bali kisomo cha "Uchambuzi/ufafanuzi chenye kupelekea kubaini herufi baada ya herufi"[4] (sana) hadi "alikuwa akisoma Surah mpaka inakuwa ndefu mno kulinganisha na Surah iliyo refu na hiyo anayoisoma (kwa kadiri inavyowezekana).[5]

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Itasemwa kwa mwenye kusoma Qur-aan (siku ya Qiyaamah): Soma na upande; soma (pole pole kwa mahadhi) kama ulivyokuwa ukisoma duniani; makaazi yako kwenye Aayah ya mwisho usomayo))[6]

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) "akirefusha kisomo chake (kwenye herufi za kurefushwa), alikuwa akirefusha Bismi Llaahi, na akirefusha Ar-Rahmaan na akirefusha Ar-Rahiym"[7]  na katika "nadhiyd" [Qaaf 50: 10][8] na mfano wa (kama) hizo.

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisimama mwisho wa kila Aayah kama ilivyoelezwa kabla.

 

Mara nyingine "alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma kwa sauti ya kuvutia ya kutetema[9] kama alviyofanya siku ya kufunguliwa kwa Makkah hali ya kuwa yuko juu ya ngamia wake, anasoma Suratul-Fat-h [48: 29] [kwa suatinyororo][10] na 'Abdullaah bin Mughaffal amesimulia hii sauti ya kuvutia : aaa"[11]

 

Alikuwa akiamrisha kuipamba sauti katika kusoma Qur-aan, alikuwa akisema: ((Ipambeni Qur-aan kwa sauti zenu (kwani sauti nzuri huzidisha kuipamba Qur-aan))[12]

 

Na alikuwa akisema: ((Hakika mwenye sauti bora miongoni mwa watu katika kusoma Qur-aan ni yule ambaye mnapomsikia akiisoma, mtamdhania ni mwenye kumkhofu Allaah))[13]

 

Alikuwa pia akiamrisha kusoma Qur-aan kwa sauti ya kupendeza, alikuwa akisema: ((Jifunzeni kitabu cha Allaah, dumisheni kuisoma, ithibitisheni (kuhifadhi), na isomeni kwa (sauti ya) kughani, kwani Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi Mwake, inakimbia haraka kuliko ngamia anavyochopoka katika kamba))[14]

 

 

Alikuwa pia akisema: ((Sio miongoni mwetu mwenye kuisoma Qur-aan bila ya kughani [kupendezesha sauti]))[15]

 

Na akisema:

((Allaah Hakuwahi kusikiliza kitu chochote zaidi ya jinsi ya kusikiliza [katika riwaaya nyingine: ((Kama Anavyomsikiliza))] Mtume (kwa shauku) ((kwa sauti ya kupendeza))], na [katika riwaaya nyingine: anavyosoma Qur-aan kwa sauti nzuri[16]  ((ananyanyua sauti kwako))[17]

 

Alimuambia Abu Muusa Al-Ash'ariyy (رضي الله عنه) ((Lau ungeliniona nilipokuwa nasikiliza kisomo chako usiku wa jana, kwa Hakika umepewa mzumari[18] katika mizumari ya aila ya Daawuud!)) Hivyo Abu Muusa akasema: "Lau ningelijua kuwa uko, ningelizidi kuitengeneza na kuipendesha sauti yangu kwa ajili yako"[19]

 

 

 

[1] Hii ni kauli ya Imaam Ash-Shaafi'y, Ahmad na Is-haaq, na pia ni rai ya baadhi ya watafiti wa Mahanafi waliokuja baadaye. Ama kuhusu kusoma Surah baada yake, huu ni mtazamo wa baadhi ya Ma-Shaafi'y na ni mtazamo Swahiyh.

[2] Al-Bukhaariy, Abu Daawuud, An-Nassaiy na Ibn Al-Jaaruud.  Na wala hii ziada sio ya pekee (haina mwenzake) (kitu kimoja hakina mwenzake hapa sio ajabu) kama At-Tuwayjiriy anavyodai.

[3] An-Nasaaiy na At-Twahaawiy ikiwa na isnaad Swahiyh.

[4] Ibn Al-Mubaarak katika Az-Zuhd (162/1 kutoka Al-Kawaakib 575), Abu Daawuud na Ahmad kwa isnaad Swahiyh.

[5] Muslim na Maalik.

[6] Abu Daawuud na At-Tirmidhiy ambaye amesema Swahiyh.

[7] Al-Bukhaariy na Abu Daawuud.

[8] Al-Bukhaariy katika Af'aal al 'Ibaad kwa isnaad Swahiyh.

[9] Inatokana na neon Tarjiy', Ibn Hajar ameeleza: kuwa ni sauti ya kutetema na asli yake ni at tardiyd, watarjiy’ sauti: ni kuikariri kutoka kwenye halq. Al-Manaawiy kasema, "Inakuja aghlabu kwa kuwa na hisia ya shangwe na furaha ambayo alikuwa  (صلى الله عليه وآله وسلم)siku  ya Ushindi wa Makkah".

[10] Al-Bukhaariy na Muslim.

[11] Al-Bukhaariy na Muslim. Ibn Hajar amesema katika maelezo kuhusu "aaa (آآآ) "hii ni hamzah ikiwa na fat-haa, ikifuatia na alif ya kimya, ikifuatia na hamzah nyingine". Shaykh 'Aliy Al-Qaariy amenukuu kama hiyo kutokana na wengine na akasema: "Ni dhahiri kuwa hizi ni Alif tatu zenye kuvutwa (ndefu)"

[12] Al-Bukhaariy ta'aliyq (kiambatisho), Abu Daawauud, Ad-Daarimiy, Al-Haakim na Tamaam Ar-Raazi kwa isnaad mbili Swahiyh.

[13] Hadiyth ni Swahiyh, imesimuliwa na Ibn Al-Mubaarak katika Az-Zuhd (162/1 kutoka Al-Kawaakib 575), Ad-Daarimiy, Ibn Naswr, At-Twabaraaniy, Abu Nu'aym katika Akhbaar Aswbahaan na Adh-Dwhiyaa katika Al-Mukhtaarah.

[14] Ad-Daarimiy na Ahmad kwa isnaad Swahiyh.

TANBIHI: Hadiyth ya kwanza imegeuzwa na msimulizi mmoja, hivyo ameisimulia: ((Pambeni sauti zenu kwa (kwenye) Qur-aan)). Haya ni makosa katika usimulizi na ufahamu, na yeyote mwenye kusema ni Swahiyh basi huyo amezama zaidi katika makosa, kwani inapingana na Simulizi Swahiyh zilizofafanuliwa katika mlango huu. Bali ni mfano bora katika Hadiyth Maqluub (iliyogeuzwa) na maelezo zaidi ya hii (tanbihi) yamo katika Silisilatul-Ahaadiyth Ad-Dhwa'iyfah (Namba 5328).

[15] Abu Daawuud na Al-Haakim ambaye amesema ni Swahiyh na Adh-Dhahaabiy amekubaliana naye.        

[16] Amesema Al-Mundhiriy ‘taghannaa’ inamaanisha kuisoma kwa sauti ya kupendeza; Sufyaan bin 'Uyaynah na wengineo wamechukua rai kwamba ni kufanya istighnaa (yaani Qur-aan kumfanya mtu ajitenge na mapambo ya dunia) lakini hii imekanushwa.

[17] Al-Bukhaariy, Muslim, At-Twahaawiy na Ibn Mandah katika Tawhiyd (81/1)

[18] Maulamaa wamesema kuwa mizumari hapa inamaansiha: sauti nzuri, na asili ya az-zumar ni al-ghinaa: kuimba, na kwamba aila ya Daawuud inakusudiwa Daawuud mwenyewe, na aila fulani hutumika na humaanisha khaswa ya mtu mwenyewe. Daawuud (عليه السلام) alikuwa na sauti nzuri mno. Hii ameitaja An-Nawawy katika maelezo yake ya Swahiyh Muslim.

[19] 'Abdur-Razzaaq katika Al-Amaaliy (2/44/1), Al-Bukhaariy, Muslim, Ibn Naswr na Haakim.

Share