06-Kukata Undugu: Vitu Vinavyosaidia Kuunga Undugu

 

VITU VINAVYOSAIDIA KUUNGA UNDUGU

 

Kuna adabu ziinazopasa kufuatwa pamoja na ndugu

 

1. Kufikiria athari zinazoendana na undugu na mwisho mzuri ni kitu kikubwa inapasa tufuatilie.

 

2. Kutazama mwisho mbaya wa ukataji undugu na hilo ni kufikiria yatakayoletwa na ukataji undugu ikiwa ni pamoja na matatizo, majuto, hasara, n.k. Ukifikiria hayo, itakusaidia uepuke kukata undugu.

 

3. Kutaka msaada kwa Allaah Kwa kumuomba Akuwezeshe katika kuunga undugu.

 

4. Kubadilisha mabaya ya ndugu kwa ihsaan. Hili linabakisha mapenzi na linahifadhi yaliyo baina ya ndugu katika makubaliano. Na linakupunguzia mwanaadamu unayopata katika ubaya wa ndugu.

 

Na kwa hilo, alikuja mtu kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) akasema: “Ewe Mtume wa Allaah, mimi nina ndugu nawaunga wananikata, nawafanyia wema na wao wananifanyia maovu, nawa mpole kwao wananifanya mjinga. Akasema “ikiwa uko kama unavyosema kanakwamba unawalisha majivu ya moto, na hutoacha kuwa unaungwa mkono na Allaah, ukidumu kwa hilo.

 

5. Kukubali udhuru wao wakikosea au kuomba msamaha.

 

Na uzuri unaotajwa katika hilo ni yaliyomfika Nabii Yuusuf na nduguze. Baada ya yote waliyomfanyia alikubali walipoomba msamaha na akawaombea Allaah Awasamehe wala hakuwagombeza kwa makosa yao.

 

6. Kuwasamehe na kusahau aibu zao hata kama hawajaomba msamaha na hilo linaonesha ukarimu wa nafsi.

 

7. Unyenyekevu na tabia laini

 

 Hilo linapelekea ndugu kumpenda mtu na kuwa karibu naye.

 

8. Kufungua macho na kutoshughulika na mambo mengine au makosa madogo sio kila uonalo unatoa kasoro, itakufanya ugombane kila mara.

 

9. Kujitolea kadri ya uwezo wako ikiwa ni cheo nafsi au mali.

 

10. Kutotaka wakusifie au wakulipe mfano wa uliyowafanyia

 

11. Kutuliza nafsi na kuridhika na kidogo kutoka kwa ndugu.

 

12. Kuchunga hali zao na kujua hisia zao na kuwaweka kuendana na daraja zao. Wako miongoni mwa ndugu mwenye kuridhia kitu kidogo, inamtosha ukimtembelea mara moja kwa mwaka, au inamtosha ukiongea naye kwa simu, mwengine inamtosha kwa ukunjufu wa uso na kuongea naye, mwengine haridhiki mpaka umzuru (umtembelee) mara kwa mara. Hivyo ishi na mtu jinsi alivyo ili ubakishe upendo.

 

13. Kuacha kuwabebesha ndugu wasiyoyaweza na kuwaondolea mazito.

 

14. Kujiepusha kulaumu sana.

 

Mpaka wazoee ndugu kumijia na kufurahi nae, mkarimu ni yule anayewapa watu haki zake na ananyamazia haki zake asipotekelezewa. Hata kukiwa na kosa inayohitaji kukemewa basi iwe kwa upole.

 

15. Kuvumilia lawama za ndugu na kuwabeba vizuri.

 

Mwenye akili na malezi mazuri anapolaumiwa na mmoja katika ndugu anachukulia vizuri na anaona anampenda, hivyo anamtaka msamaha kupunguza hasira zake na inaonesha anataka amtembelee ndio maana analaumu.

 

16. Kuwa kati na kati katika mizaha na ndugu kuchunga hali zao na kujiepusha kuwatania wasiopenda hilo.

 

17. Kujiepusha na ugomvi na majadiliano mengi haya yote inarithisha bughdha, ubinafsi na inachafua mahusiano.

 

18. Kuharakisha kuwapa zawadi ikitokea migongano na ndugu. Zawadi zinaleta upendo na kuepusha dhana mbaya.

 

19. Aweke akilini mwanaadamu kwamba ndugu ni pande la nyama kutoka kwake kwa hiyo hana budi kuwa nao wala hawezi kujivua wakitukuka wao ndio kutukuka kwake wakidhalilika ndio kudhalilika kwake.

 

20. Ajue kuwa kuwafanyia uadui ndugu ni shari na balaa mwenye kufaidika kwa hili ni mwenye hasara na mwenye kushinda ni mwenye kushindwa.

 

21. Kuchunga katika kuwakumbuka ndugu katika sherehe na matukio mbalimbali. inatakiwa mtu aandike majina na namba za simu za ndugu na azihifadhi ili iwe rahisi kuwakumbuka anapowahitaji. Na anapomsahau mmoja wao amwendee amwombe msamaha na amridhishe kadri ya uwezo wake.

 

22. Kupupia kupatanisha.

 

Inapasa aliyepata bahati ya kupendwa katika familia arekebishe panapotokea matatizo kwani mzozo usiposuluhishwa moto wake utawaenea wote.

 

23. Kuharakisha kugawa mirathi.

 

Ili kila mmoja achukue fungu lake na kusienee ugomvi na madai na kuwe na mafungamano baina ya ndugu.

 

24. Kupupia uhusiano mzuri na maafikiano katika ushirika.

 

Wakiingia ndugu katika kushirikiana kila mmoja achunge waelewane katika mambo yao na yawe na kujitolea na upendo kushauriana na kuhurumiana ukweli na amana na kila mmoja ampendelee mwenzie analopendelea nafsi yake na kila mtu ajue wajibu wake na wa mwenzie.

Kama inavyopendezwa wajadiliane matatizo kwa uwazi wapupie kufikia muafaka na ikhlaas katika kazi na kusamehe vitu vidogo, pia waandike maafikiano yao.

 

25. Mikutano ya mara kwa mara.

 

Iwe kila mwezi au mwaka kukutana huku kuna kheri nyingi watu wanajuana, wanaungana, wanapeana naswaha na haswa haswa wasimamizi wakiwa ni wenye elimu.

 

26. Sanduku la wanandugu.

 

Ambalo hukusanywa michango ya ndugu yenye wasimamizi katika familia ili atakapohitaji mmoja katika wanafamilia mali kwa ajili ya ndoa au lingine wanafanya haraka kujua hali yake na kumsaidia; hili linazalisha mapenzi na kuikuza.

 

27. Kielekezo cha ndugu.

 

Inapendeza baadhi ya ndugu waweke kielekezo maalum ndani yake kuna namba za ndugu za simu kisha ichapishwe na kugawanyiwa ndugu wote, hili linasaidia kuwaunganisha na inamkumbusha mtu ndugu zake akitaka kuwasalimia au kuwaita katika mjumuiko na harusi.

 

28. Tahadhari na kuwatia uzito ndugu.

 

Na hilo ni kuwa mbali na kila sababu inayopelekea hilo, unajiepusha na kuwatia uzito wasiokuwa na uwezo na usiwalaumu kwa wasiyoyaweza.

 

29. Mashauriano baina ya ndugu

 

Inapendekezwa kwa ndugu kuwa na kikao cha majadiliano au kuwa na viongozi watakaowaendea wakati wa tatizo ili wapate wazo moja na linalomridhisha Allaah, inatakiwa viongozi hao wawe wapole wenye uoni na rai nzuri.

 

30. Mwisho ichungwe katika hilo, uwe undugu unawakaribisha kwa Allaah kwa ikhlaas bila kumshirikisha na kuwe kusaidiana katika wema na Uchamungu. Isikusudiwe ujinga wa kijahilia.

 

Mwisho tunamshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na kumtakia rehma na amani Mtume wetu.

 

Pia nachukua fursa hii kuwashukuru wote waliosaidia katika kupitia.

 

 

Ndugu msomaji unaruhusiwa kutuma maoni na kurekebisha panapostahili Ukamilifu ni  wa Allaah pekee, na kama tunavyofahamu upana wa Lugha ya Kiarabu na ufinyu wa Lugha ya kiswahili.

 

Share