Anaweza Kuswali Katika Nyumba Ya Asiye Muislamu?

Anaweza Kuswali Katika Nyumba Ya Asiye Muislamu?

 

 

SWALI:

 

Assalaam aleikum.

 

Kwanza nimefurahi sana kuipata website hii mola awabariki.

swali langu ni hili.mimi nafanya kazi za nyumbani katika nyumba za wazee wasiokua waisilamu,wakati wakuswali huswali katika nyumba hio.je yafaa kuswali au haifai hata kama hapana najisi kwa vile mwenye nyumba hio simuislamu na ameridhika ni swali bila tabu?

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Unaweza kuswali katika nyumba hiyo ikiwa una dharura na madamu tu ni mahali pasafi hakuna najsi na hakuna picha au misalaba mbele yako.

 

  

Kwa maelezo zaidi bonyeza kiungo kifuatacho:

 

Swalah Katika Kanisa Inafaa?

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share