036-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kurefusha Kisimamo Hiki Na Wajibu Wa Kutulia Ndani Yake

 

 

KUREFUSHA KISIMAMO HIKI NA WAJIBU WA KUTULIA NDANI YAKE 

 

Alikuwa   (صلى الله عليه وآله وسلم) akikifanya kisimamo chake hiki kuwa kirefu, (kama) unaokaribiana na urefu wa rukuu yake kama ilivyotajwa; bali, alikuwa akisimama mara nyingine mpaka msemaji husema: "Amesahau" [kutokana na kusimama kwake muda mrefu]".([1])

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akiamrisha (wafanye) utulivu humo. Alimwambia aliyeswali vibaya ((…kisha nyanyua hadi unyooke sawa sawa hali ya kuwa umesimama (kila mfupa urudi mahali pake) [katika riwaaya nyingine] Unapoinuka nyoosha uti wako na nyanyua kichwa chako hadi mifupa irudi katika viungo vyake))([2]). Pia alimkumbusha kwamba: ((Swalah ya mtu haitimii kama hajafanya hivyo)).

 

Na alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Allaah عزوجل Hatazami Swalah ya mja asiyenyosha uti wake wa mgongo barabara baina ya rukuu zake na sijda zake)).([3])

 

 

 





[1] Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad. Imetolewa katika Al-Irwaa (namba 307).

[2] Al-Bukhaariy, Muslim, Ad-Daraamiy, Al-Haakim, Ash-Shaafi'iy na Ahmad.

TANBIHI: Maana ya Hadiyth hii iko dhahiri na wazi, nayo ni utulivu katika kusimama huku. Ama utumiaji wa Hadiyth hii unaofanywa na baadhi ya ndugu zetu katika watu wa Hijaaz na kwengineko kama ni dalili ya kuthibitisha kuweka mkono wa kulia juu ya kushoto katika kusimama, bila shaka iko  mbali sana na  riwaaya nyingi za Hadiyth. Bali ni hoja ni batili, kwani uwekaji uliotajwa, haukuja utajo wake katika kisimamo cha kwanza katika usimulizi wowote ule wa Hadiyth na katika matamshi yake (Hadiyth). Basi inakuaje kupelekea kutafsiri "mifupa irudi sehemu yake" iliyotajwa katika Hadiyth kuwa ni mkono wa kulia kuukumata mkono wa kushoto kabla ya rukuu?! Hii ingelitumika kama matamshi yote ya Hadiyth yangeasiriwa kumaanisha hivi. Basi vipi kuhusu wanavyohusisha maana iliyobainisha maana tofauti kabisa? Bali kuweka kwake hakuwezi kufahamika kutoka katika Hadiyth kabsia, kwa vile iliyokusudiwa 'mifupa' ni mifupa ya uti wa mgongo, kama ilivyothibitishwa katika Sunnah, "…alikuwa akisimama kwa kunyooka barabara hadi kila mfupa ulirudi sehemu yake."

 

Mimi binafsi, sina shaka kwamba kuweka mikono juu ya kifua katika kusimama ni uzushi unaopotoa, kwani haikutajwa katika Hadiyth zozote za Swalah juu ya kwamba ni nyingi mno. Ingelikuwa kutendeka huko kuna asili, ingelitufikia japo katika usimulizi mmoja. Juu ya hivyo, hakuna hata Salaf mmoja aliyefanya hivyo, wala hakutaja hata mmoja wa Maulamaa wa Hadiyth nijuavyo.

 

Hii hailingani na alivyonukuu Shaykh At-Tuwayjiriy katika Makala yake (Uk. 18-19) kutoka kwa Imaam Ahmad (رحمه الله), "Akipenda mtu, anaweza kuacha mikono yake pembeni, au akipenda anaweza kuweka kifuani mwake", kwani Imaam Ahmad hakuhusisha hii kwa Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم), bali alisema kutokana na ijtihaad  na rai yake mwenyewe. Na rai inaweza kuwa imekosewa. Inapopatikana dalili sahihi dhidi ya uzushi inafuatwa na kuachwa hiyo ya uzushi, mfano kama hii, hivyo kauli ya Imaam yenye mapendekezo yake haikanushi uzushi wake kama alivyoandika Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyah (رحمه الله). Bali naona haya maneno yake ni ishara kwamba Imaam Ahmad hakuchukulia kuwekwa kulikotajwa juu kama ni kumethibitika katika Sunnah, kwani ameruhusu uchaguzi baina ya kutenda na kuacha kutenda. Je, anadhani Shaykh Mheshimiwa kwamba Imaam aliruhusu pia uchaguzi kuhusu uwekaji wa mikono kabla ya rukuu? Hivyo imethibitika kwamba kuweka mikono kifuani katika kusimama baada ya rukuu sio katika Sunnah. Haya ni majadiliano mafupi ya mas-ala haya  ambayo yanaweza kujadiliwa katika maelezo zaidi kwa upana, lakini kutokana na uchache wa sehemu hapa, inatosha, na badala yake, ni ubainisho wangu dhidi ya Shaykh (At-Tuwayjiriy) katika Chapa ya tano (Uk. 30) chapa mpya.

 

     

[3]    Ahmad na Atw-Twabaraaniy katika Mu'jam Al-Kabiyr ikiwa na isnaad Swahiyh.

Share