Kumfanyia Mtoto Sherehe Anapomaliza Kusoma Au Kuhifadhi Qur-aan

 

Kumfanyia Mtoto Sherehe Anapomaliza Kusoma Au Kuhifadhi Qur-aan

 

Alhidaaya.com

 

 

 SWALI:

 

 

Assalaam aleykum .nimeambiwa na ustaadh kwamba ni lazima nimfanyie mwanangu sherehe ya kumaliza juzuu.je kuna ulazima au umuhimu wa kufanya hili jambo?

Shukran!

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Hakuna dalili ya jambo hilo. Ustaadh aliyelazimisha jambo hilo ingelikuwa vyema kama angelikupa dalili kutoka katika Qur-aan au Sunnah kwani ‘amali zetu za Dini zote zinatokana na nyanzo hizo mbili. Na kwa vile hakuna dalili ya jambo hilo, basi linabakiwa jambo hilo kuwa ni la kuzushwa lisilokuwa la kweli na inapasa kujiepusha nalo.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share