Qur-aan Ina Suwrah Ngapi Na Aayah Ngapi Jumla?

 

Qur-aan Ina Suwrah Ngapi Na Aayah Ngapi Jumla?

 

Alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Qur ani ina aayah ngapi na mna suwrah ngapi

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Jumla ya Suwrah za Qur-aan ni 114 kuanzia Suwrah Al-Faatihah hadi Suwrah An-Naas. Majina yake na idadi zake imetajwa   

 

katika kurasa za Mswahafu mwisho kabisa.

 

 

Ama idadi za Aayah, wengine wamesema ni 6666, lakini iliyo sahihi kabisa ni ya  Aayah  6,236.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

 

 

Share