Anafanya Kazi Ya Kuchunga Watu Wasizame – Kuna Wanawake Wako Uchi Je, Halali Au Haramu?

SWALI:

Assalam aleikum awrahmatullah wabarakaatuh?

Ama baada ya salam, mim ni kijana ambae nafanya kazi hotelini, kazi yangu ni kuchunza wageni wasizame katika mahali pa kuogelea. Na wageni hao huvaa uchi (sidiria na chupi) wanawake. Jee yafaa kufanya kazi hiyo? Na pato langu ni halali ama haramu? Shukran


  

JIBU:

AlhamduliLLaah - Sifa njema zote Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kuchunga wanawake walio uchi wasizame.

 

Kazi hiyo si sawa kufanywa na kijana Muislamu kwa kuwa kazi hiyo ni kuokoa wanawake walio uchi pindi wanapokuwa wanazama. Mpango ulio mzuri katika kazi hiyo ni mwanaume kuwaokoa wanaume, na mwanamke awepo wa kufanya kazi hiyo ya kuwaokoa wanawake wenzake.

 

Uharamu wa mwanaume kufanya kazi hiyo ni kule kuwepo katika eneo lililo na wanawake wasiojistiri vizuri. Linalotakiwa ni wewe uzunguze na wenye hoteli ikiwa ni Waislamu inaweza kuwa rahisi lakini hata ikiwa si Waislamu uwaelezee hilo na huenda wakakufahamu na kukupatia kazi mbadala.

 

Ikiwa mwenye hoteli hakukubali itabidi ufanye juhudi ya kutafuta kazi nyingine. Na uache hiyo pindi tu unapofanikiwa katika hilo lakini ni lazima ujiwekee muda na ufanye bidii. Ukifanya hivyo basi Allaah Aliyetukuka Atakusaidia inshaAllaah.

 

Tunakuombea kila la kheri katika suala hilo.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share