016-Unawezaje Kuupata Moyo Wa Mumeo Na Kumridhisha Mola Wako: Kutekeleza Ahadi Ni Katika Sifa Za Manabii

 

KUTEKELEZA AHADI NI KATIKA SIFA ZA MANABII

 

Kuwa mwadilifu kwa mume wako, na usikufuru namna mnavyoishi naye, na usisahau fadhila mlizofanyiana, kwa hakika haya yanatokana na uzuri wa uangalizi wako wa nyumba yako na kuihifadhi nyumba yako, nayo hupelekea kuokoka na moto.

 

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema kuwaambia wanawake,

“Toeni sadaka kwa wingi kwani wengi wenu mtakuwa kuni za motoni!! Mwanamke akauliza, Je, ni kwa sababu gani? Mtume akasema, ‘Kwa sababu hamuachi kulalama sana na mnakufuru maisha yenu ya ndoa, baada ya hapo wakawa wanatoa sadaka vidani vyao na kuweka katika nguo ya Bilaal (Radhiya Allaahu ‘anhu)”[1]

 

Kukufuru ndoa maana yake kutotekeleza ahadi, ikiwa mume ameweza kuishi vizuri na mke wake muda wote lakini ikatokezea siku moja akamkosea basi atasahau ihsani aliyofanyiwa muda wote uliopita na atasema, ‘Hakuna hata siku moja aliyonifanyia mema’. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa mtu mwadilifu zaidi na hata baada ya kifo cha mke wake Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha), kwa ajili ya Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha) Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwakirimu marafiki wa Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha) na akiwatembelea mara kwa mara, ilipotokezea kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anha) kumuonea wivu Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha), Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anha) akimwambia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa, Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha) alikuwa mwanamke mzee na Mwenyezi Mungu Amembadilishia kilicho bora zaidi yake (yaani Mtume akapewa  Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anha) baada ya kifo cha Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha). Mtume akamjibu Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anha) kwa kusema, ‘WAllaahi, Mwenyezi Mungu Hakunibadilishia kilicho bora ya Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha).’ Hadiyth hii imetajwa hapo nyuma, baada ya hapo Mtume akawa anamtajia Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anha) fadhila za Mama wa Waumini Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘anha).

 





[1] Imepokewa na Al-Bukhaariy

Share