Kutumia Huduma Za Wireless Internet Ikiwa Hujui Ni Ya Nani; Je Itakuwa Ni Kumuibia Mtu?

 

SWALI:

 

assalam  alaykum  shehe naanza kwa kuwapongeza  kwa  kuanzisha hii website  inasaidia  sana  hasa kwa sisi tulio mbali na  nchi yetu  kwa kuufahamu  uislamu  vizuri  na  makini mahala  nilipo  ni  kuna  wireless intenet  nyingi ila  nyingi  ni  za watu  binafsi  na  zina  password  ila  chache  hazina  na  zingine  ni  za umma kuzitofautisha  kwamba  hii ni  ya  mtu binafsi  na  hii ni  ya umma ni  ngumu  na  hata  hivyo  wahusikA wa hizi  intanet  ni  vigumu  kuwajua je  nikitumia kuna  makosa?  Ni hayo tu waleikum msallaam

 


 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola  wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kutumia huduma za wireless internet ikiwa humjui mwenyewe.

 

 

Ikiwa zipo wireless nyingi namna hiyo na wewe unaweza kwenda kwa wahusika ukapata ya kwako, kwani kutumia ya mtu mwengine ikiwa unamjua au humjui ni makosa na ni wizi. Sababu ni kuwa wenyewe wanalipia huduma hiyo na ikiwa nawe utaunganisha na kuanza kutumia huduma hiyo utaongeza gharama hata kama ni ndogo, au kuzoretesha huduma yake na kuifanya isiwe na kasi kama kawaida. Na wizi wa aina yoyote japo mdogo au usiohisika haukubaliwi katika Dini yetu.

 

Hivyo, jiepushe kabisa katika utumiaji wa internet hizo.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share