Mandi Na Nyama (Yemen)

Mandi Na Nyama (Yemen)

 

Vipimo

Mchele - 3 Magi

 Nyama ya mafupa - 2 Ratili (LB)

Mafuta - ¼ kikombe

Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa - 3 kikubwa

Bizari ya pilau ya unga (cumin) - 1 kijiko cha chakula

Pilipili manga -  ½ kijicho cha chai

Hiliki - ½ kijiko cha chai

Karafuu ya unga - ¼ kijiko cha chai

Mdalasini nzima - 3 Vijiti

Mdalasini   wa unga - ½ kijiko cha chai

Kitunguu saumu na tangawizi - 2 vijiko vya chakula

Nyanya iliyokatwakatwa - 1 nzima

Kidonge cha supu - 1 au 2

Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji - 1 kijiko cha chai

Zabibu kavu (ukipenda) - ¼ kikombe

Pilipili mbichi - ukipenda

Chumvi - kiasi

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Kwenye sufuria katakata  nyama  naisafishe vizuri kisha tia binzari zote pamoja na vitunguu viwili,  nyanya freshi, thomu na tangawizi na chumvi kiasi acha ichemkie huku ukiongeza maji mpaka iwive vizuri.
  2. Ikishawiva epua nyama zote tia kwenye treya ya kuchomea kisha ukipenda unaweza kuongezea viungo au hivyohivyo ukaichoma (bake) kwa moto wa 350° C mpaka rangi ibadilike.
  3. Ile supu inayobaki ichuje vizuri weka kando kwa ajili ya kupikia wali.
  4. Tia mafuata katika sufuria, kisha kaanga tena kitunguu kimoja tia mdalasini kidogo na thomu na tangawizi na kidonge cha supu 1 au 2 acha ikaangike kisha mimina ile supu, ukipenda unaweza kutia rangi ya zafarani au rangi ya biriani acha ichemke kisia maji kutokana na mchele, kisha mimina mchele  upike mpaka uwive.
  5. Ukishawiva pakua kwenye sahani kisha weka nyama yako juu ya wali tayari kwa kuliwa na saladi au pilipili.

 

Kidokezo:

   Ukipenda unaweza kutia zabibu kavu kwenye wali.

  Tolea na kachumbari yake.

 

Share