03-Wasifu Wa Maswahaba Kumi Waliobashiriwa Pepo: Utangulizi

 

Utangulizi

 

Roho ya binadamu hujitahidi kupata furaha kwa juhudi zote. Kwa bahati mbaya watu wanapokuwa katika juhudi hizo hupata matatizo na maafa. Na haya hujiri mtu anapoacha kufuata mwongozo wa Uislamu na hasa kwa mtu anayedhani kuwa kiasi kubwa cha mali ndio utatuzi wa mikasa aliyonayo. Mwana falsafa mkubwa aliyeitwa Aristotle alisema kuwa furaha inapatikana kupitia tafakuri juu ya Mungu (Allaah) na kwa kuishi maisha yenye nidhamu. Hapana maelezo mazuri juu ya Uislamu kuliko kauli isemayo, “Kuwa ni Njia ya maisha yenye Nidhamu.”

 

Maswahaba wa Mjumbe wa Allaah walikuwa watambuzi wa ukweli huu. Hivyo, walimridhisha Allaah, na kufanya hivyo, walipata furaha na maendeleo katika maisha yao. Katika jumuiya ya Kiislamu, utajiri unagawanywa. Wale wenye kingi wanagawana kingi, na wale wahitaji wanapewa sehemu. Tunapomridhisha Allaah, mizani zetu za amali njema zinajaa na Pepo ndio tuzo yetu siku ya Hesabu. Je, kuna tuzo na mahali bora zaidi kuliko Peponi?

 

Jihadi inaweza kuwa tukio la kila siku, Maswahaba walikuwa wapanda farasi mchana na jioni waliitumia kufanya ibada. Walikuwa watu wa kusali, kufunga, kutoa sadaka, wakarimu wa kweli. Waliokuwa safi (wasiofanya dhambi), waaminifu na wacha-Mungu. Walikuwa watu waliomudu kudhibiti fikra zao, mwili na hasira. Hawakuridhisha utashi wa nafsi zao. Walijishughulisha kuwalisha wenye njaa. Yote tuliyo yadhukuru ni Jihadi.

 

Mwito wa Jihadi (yaani vita au mapambano) uliponadiwa, Maswahaba walikuwa tayari wamejitolea muhanga kwa kila kitu; mali zao, maisha yao, na waliziacha familia zao majumbani.

 

Hawakuogopa kifo kwa sababu hawakujua njia bora ya kufa zaidi ya kupigana kulinda haki za Kiislamu au maadili yaUislamu.

 

Na hii ndio maana halisi ya shahada, La ilaaha illa Allaah (hapana apasae kuabudiwa ila Allaah), Allaah aliwaruzuku furaha ya kweli na Pepo kama malipo ya uaminifu katika njia yake.

 

Pepo ni makazi ya mwisho na ya kudumu ya waumini na wacha-mungu. Kuna Maswahaba wengi waliobashiriwa Pepo kwa kutambua ibada zao na hadhi ya juu.  Tunapo kitalii kitabu hiki tutapata fursa ya kujifunza habari zao. Na kwa kufanya hivyo tutajifunza njia ya kwenda Peponi.

 

Share