Vitumbua Vya Shira

Vitumbua Vya Shira

 

 

Vipimo

Unga - 2 gilasi

Mayai - 4

Hamira - 2 vijiko vya chai 

Maziwa ya maji - 2 gilasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Weka mayai katika bakuli kisha yapige vizuri.
  2. Tia maziwa koroga.
  3. Tia hamira, koroga.
  4. Tia unga uchanganye vizuri.
  5. Weka uumuke, ukiwa tayari choma/pika kama unavyopika vitumbua vya kawaida.
  6. Vikishapoa weka kwenye sinia na mimina shira vikiwa tayari kuliwa.

Shira:

Sukari - 1 gilasi

Maji - 2 gilasi

ladha - hiliki au arki (rose flavour) n.k - 5 matone

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Weka vitu vyote pamoja katika sufuria uweke motoni ichemke kidogokidogo hadi iwe tayari. Isiwe nzito, bali nyepesi.
  2. Tia ladha, iache ipowe na kuwa tayari kumiminwa juu ya vitumbua.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Share