06-Swalaah – Kuwajibika Na Fadhila Zake: Fadhila Za Swalah

Swalaah – Kuwajibika Na Fadhila Zake

 

06-Swalaah – Kuwajibika Na Fadhila Zake: Fadhila Za Swalaah

 

Alhidaaya.com

 

 

Fadhila za Swalaah ni nyingi na tukufu mno, lau kila Muislamu atazitambua na kuzipima uzito wake, basi hakuna atakayetaka kuzikosa. Tumebashiriwa fadhila zake katika Aayah na Hadiyth nyingi, miongoni mwazo ni:

 

 

1- Swalaah inabashiria kumwepusha Muislamu kutokana na machafu na maovu na hufutiwa madhambi:  

 

 اتْلُ مَا أُوحِيَ إِلَيْكَ مِنَ الْكِتَابِ وَأَقِمِ الصَّلَاةَ ۖ إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ

Soma (ee Muhammad Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) uliyoletewa Wahy katika Kitabu na simamisha Swalaah, hakika Swalaah inazuia machafu na munkari. [Al-‘Ankabuwt: 45]

 

 

 Na Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((أَرَأَيْتُمْ لَوْ أَنَّ نَهْرًا بِبَابِ أَحَدِكُمْ يَغْتَسِلُ مِنْهُ كُلَّ يَوْمٍ خَمْسَ مَرَّاتٍ هَلْ يَبْقَى مِنْ دَرَنِهِ شَيْءٌ؟)) قَالُوا: لَا يَبْقَى مِنْ دَرَنِهِ شَيْءٌ. قَالَ: ((فَذَلِكَ مَثَلُ الصَّلَوَاتِ الْخَمْسِ يَمْحُو اللَّهُ بِهِنَّ الْخَطَايَا))     رواه البخاري ومسلم

 

Amesimulia Abuu Hurayrah (رضي الله عنه): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:Mnaonaje kungekuwa na mto mlangoni mwa mmoja wenu na akaoga mara tano kwa siku. je, atabakiwa na tone la uchafu (mwilini mwake)?”  Wakasema: “Hatabakiwa na tone la uchafu.” Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ”Basi hivyo ni mfano wa Swalaah tano ambazo Allaah Anafuta madhambi kwazo.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Na pia Hadiyth ya:

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ ((الصَّلَاةُ الْخَمْسُ، وَالْجُمْعَةُ إِلَى الْجُمْعَةِ، كَفَّارَةٌ لِمَا بَيْنَهُنَّ، مَا لَمْ تُغْشَ الْكَبَائِرُ)) رواه مسلم

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swalaah tano na Ijumaa hadi Ijumaa ni kafara baina yao madamu hayafanywi Al-kabaair [madhambi makubwa])) [Muslim]

 

 

Pia:

 

 

عَنْ عُثْمَانَ بْنِ عَفَّانَ، قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((مَنْ تَوَضَّأَ لِلصَّلَاةِ فَأَسْبَغَ الْوُضُوءَ، ثُمَّ مَشَى إِلَى الصَّلَاةِ الْمَكْتُوبَةِ، فَصَلَّاهَا مَعَ النَّاسِ أَوْ مَعَ الْجَمَاعَةِ أَوْ فِي الْمَسْجِدِ غَفَرَ اللهُ لَهُ ذُنُوبَه)) مسلم

Kutoka kwa ‘Uthmaan bin ‘Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Atakayetawadha kwa ajili ya Swalaah, akafanya vizuri wudhuu wake kisha akaenda kuswali Swalaah za fardhi akaziswali pamoja na watu au jamaa au Msikitini Allaah Atamfutia madhambi yake)) [Muslim]

 

 

 

2- Swalaah inabashiria kwamba ni nuru:

 

  (( الصلاة نور)) رواه مسلم والترمذي

 

((Swalaah ni nuru)) [Muslim na At-Tirmidhiy

 

 

 

3-Swalaah inabashiria kupandishwa daraja na kufutiwa dhambi kwa kila sajdah moja:

 

 

 ‏‏((ما مِن عبدٍ يسجدُ للَّهِ سَجدةً إلَّا كتبَ اللَّهُ لَهُ بِها حسنةً، ومحا عنهُ بِها سيِّئةً، ورفعَ لَهُ بِها درجةً، فاستَكْثروا منَ  السُّجُود))   رواه ابن ماجه

((Mja yeyote atakayesujudu sajda moja ataandikiwa wema mmoja, na atafutiwa baya moja, na atapandishwa daraja yake, kwa hiyo, zidisheni kusujudu)) [Ibn Maajah]  

 

 

 

4-Swalaah inabashiria kumuingiza Muislamu Jannah:

 

 

 عن أَبِي موسى الأشعرِيِّ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّه صلى الله عليه وسلم: ((منْ صلَّى الْبَرْديْنِ دَخَلَ الْجنَّةَ)) متفقٌ عَلَيهِ

Kutoka kwa Abuu Muusa kwamba Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((AtakayeswaliAl-Bardayn (Swalaah ya Alfajiri na 'Ishaa) ataingia Jannah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

5- Swalaah inabashiria kuwa karibu na Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) huko Jannah:

 

 

 عن أبي فراس رَبِيعَة بْن كَعْبٍ الْأَسْلَمِيُّ رضي الله عنه    خادم رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: كُنْتُ أَبِيتُ مَعَ رَسُولِ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَأَتَيْتُهُ بِوَضُوئِهِ وَحَاجَتِهِ، فَقَالَ لِي: ((سَلْني)) فَقُلْتُ: أَسْأَلُكَ مُرَافَقَتَكَ فِي الْجَنَّةِ، قَالَ: ((أَوْ غَيْرَ ذَلِكَ؟))  قُلْتُ: هُوَ ذَاكَ، قَالَ: ((فَأَعِنِّي عَلَى نَفْسِكَ بِكَثْرَةِ السُّجُودِ)) رواه مسلم في  صحيحه

Kutoka kwa Abuu Firaas Rabiy'ah bin Ka'ab Al-Aslamiy mtumishi wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye amesema: "Nililala na Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) usiku mmoja nikamletea maji ya kutawadha, akaniambia: ((Niombe utakacho)) Nikasema: "Nataka kuandamana na wewe Jannah. Akasema: ((Hutaki lolote lingine?)) Nikasema: "Ni hilo tu."  Akasema:  ((Basi nisaidie (ili hilo liwezekane) kwa kuzidisha kusujudu [Kuswali])) [Muslim katika Swahiyh yake] 

 

 

6-Swalaah inabashiria kuombewa Rahmah na Malaika:

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((المَلاَئِكَةُ تُصَلِّي عَلَى أَحَدِكُمْ مَا دَامَ فِي مُصَلَّاهُ الَّذي صَلَّى فِيه مَا لَمْ يُحْدِثْ تُقُول: اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ، اللَّهُمَّ ارْحَمْهُ))  متفق عليه

 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Malaika wanamswalia mmoja wenu madamu amebakia sehemu aliyoswali ikiwa hakutengua wudhuu wake, (Malaika) Husema:  "Ee Allaah! Mghufurie, Ee Allaah Mrehemu.")) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

7-Swalaah inabashiria kubakia katika kuhifadhiwa na Allaah:

 

عن جندب بن عبدالله رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَن صَلَّى الصُّبحَ فَهُوَ فِي ذِمَّةِ اللَّهِ...))  مسلم (657)

 

Kutoka kwa Junub bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayeswali asubuhi atakuwa katika hifadhi ya Allaah)) [Muslim]

 

 

 

8-Swalaah inabashiria kufutiwa madhambi yaliyotangulia:

 

 

عن أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِذَا قَالَ أَحَدُكُمْ آمِينَ وَقَالَتْ الْمَلَائِكَةُ فِي السَّمَاءِ آمِينَ فَوَافَقَتْ إِحْدَاهُمَا الْأُخْرَى غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ)) متفق عليه

 ((Atakaposema mmoja wenu (katika Swalaah) Aamiyn, na Malaika mbinguni wakasema Aamiyn, zikawafikiana pamoja, atafutiwa madhambi yake yaliyotangulia)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 Pale Waumini wanaposema: “Aamiyn” baada ya kusomwa Suwratul-Faatihah.

 

 

9-Swalaah inabashiria kujiepusha na unafiki:

 

  عن أَبي هُريرة رضيَ اللَّه عنهُ   قال : قال رسولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : (( لَيْسَ صَلاةٌ أَثْقَلَ عَلَى المُنَافِقينَ مِنْ صلاة الفَجْرِ وَالعِشاءِ وَلَوْ يَعْلَمُونَ ما فِيهما لأَتَوْهُما وَلَوْ حبْوًا)) متفق عليه .

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakuna Swalaah iliyo nzito kwa wanafiki kama Swalaah ya Alfajiri na ‘Ishaa. Lau kama wangelijua yaliyomo humo (fadhila na faida) wangeliziendea (kuziswali) japo kwa kutambaa)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Azidi kutuzindua na Atuzidishie iymaan na tawfiyq ya hidaaya tutekeleze ‘ibaadah hii tukufu ili tutimize nguzo hii adhimu ya Kiislamu na tujaaliwe kuchuma thawabu na fadhila nyingi za Swalaah. Na tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Atutakabalie Swalaah zetu, na tusiache kuomba du’aa Baba yetu Nabiy Ibraahiym ('Alayhis-Salaam) ili tuwe wenye kusimamisha Swalaah pamoja na vizazi vyetu:

 

رَبِّ اجْعَلْنِي مُقِيمَ الصَّلَاةِ وَمِن ذُرِّيَّتِي ۚ رَبَّنَا وَتَقَبَّلْ دُعَاءِ﴿٤٠﴾

 “Rabb wangu! Nijaalie niwe mwenye kusimamisha Swalaah na dhuria wangu. Rabb wetu! Nitakabalie du’aa yangu.” [Ibraahiym: 40]

 

 

 

 

 

 

Share