07-Wewe Pekee Tunakuabudu: Yanayokubalika Katika Du’aa

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

07- Yanayokubalika Katika Du’aa

 

 

Baadhi ya yanayokubalika katika kuomba du’aa na dalili zake:

 

 

1- Kuzidisha Du’aa

 

Inakubaliwa kuomba du’aa kwa wingi kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ni Mkarimu mno na Mwingi vipawa, fadhila na kutunuku. Dalili ni Hadiyth ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘Anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

((إذَا سَألَ أحَدَكَمُ فَلْيُكْثِر، فَإنَّمَا يَسْألُ رَبَّهُ))

((Anapoomba mmoja wenu basi azidishe [du’aa] kwani anamuomba Rabb wake)) [Ibn Hibbaan - Swahiyh Al-Jaami’ (591)]

 

Pia katika riwaayah nyingine Hadiyth ya ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa):

 

(( إِذَا تَمَنَّى أحَدَكَمُ فَلْيُكْثِر، فَإنَّمَا يَسْألُ رَبَّهُ))

((Atakapotamani mmoja wenu basi azidishe [du’aa] kwani anamuomba Rabb wake)) [Atw-Twabaraaniy - Swahiyh Al-Jaami’ (437)]

 

 

 

2- Kuangaza Juu Wakati Wa Kuomba Du’aa

 

‘Ulamaa wamekubaliana kwamba inakubalika kuangaza juu wakati wa kuomba du’aa anapokuwa mtu nje ya Swalaah. Dalili mojawapo ni pale alipokuwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiaga dunia akanyanyua macho yake kutazama juu na kusema:

 

((الرَّفِيقِ الأَعْلَى فِي الرَّفِيقِ الْأَعْلَى))

(([Niwe na ] Rafiki wa juu, kwa rafiki wa juu)) [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad katika riwaaya mbali mbali]

 

Pia katika kisa cha Miqdaad (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kuhusu kinywaji cha maziwa alichokunywa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) bila ya kujua kwamba kinatoka kwake. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipofika Msikitini na kumaliza kuswali alikiendea kinywaji akanywa kisha akainua kichwa chake kuangaza juu na kuomba:

 

((اللَّهُمَّ أَطْعِمْ مَنْ أَطْعَمَنِي وَأَسْقِ مَنْ أَسْقَانِي))

((Ee Allaah, mlishe aliyenilisha, na mnywishe aliyeninywesha)) [Muslim na Swahiyh Muslim (2055)]

 

Pia,

 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) قَالَ: رَأَيْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) جَالِسًا عِنْدَ الرُّكْنِ،  فَرَفَعَ بَصَرَهُ إِلَى السَّمَاءِ فَضَحِكَ، فَقَالَ: ((لَعَنَ اللَّهُ الْيَهُودَ ثَلاَثاً، إِنَّ اللَّهَ حَرَّمَ عَلَيْهِمْ الشُّحُومَ فَبَاعُوهَا، وَأَكَلُوا أَثْمَانَهَا، وَإِنَّ اللَّهَ إِذَا حَرَّمَ عَلَى قَوْمٍ أَكْلَ شَيْءٍ حَرَّمَ عَلَيْهِمْ ثَمَنَهُ))

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nilimuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa ameketi pembeni akanyanyua macho yake mbinguni akacheka kisha akasema: ((Allaah Awalaani Mayahudi,  (mara tatu), hakika Allaah  Amewaharamishia shahamu  wakaiuza kisha wakala thamani yake. Na hakika Allaah Anapoharamisha kwa watu kula kitu Ameharamisha pia thamani yake)) [Abuu Daawuwd na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (3488)]

 

Lakini katika Swalaah imekatazwa kuangaza juu kwa dalili kadhaa mojawapo ifuatayo:  

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لَيَنْتَهِيَنَّ أَقْوَامٌ عَنْ رَفْعِهِمْ أَبْصَارَهُمْ عِنْدَ الدُّعَاءِ فِي الصّلاَةِ إِلَى السَّمَاءِ أَوْ لَتُخْطَفَنَّ أَبْصَارُهُمْ))

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Watu lazima waache kutazama juu mbinguni katika Swalah au macho yao yatanyofolewa)) [Muslim, An-Nasaaiy ameisahihisha Al-Albanaiy katika Swahiyh An-Nasaaiy (1275), Swahiyh Al-Jaami’ (5479)

 

 

3- Kuwaombea Wasio Waislamu 

 

Inafaa kuwaombea wasio Waislamu du’aa nzuri au mbaya kwa kutegemea na hali au sababu zake. Mfano inafaa kuwaombea wazazi hidaaya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Awaongoze katika Uislamu. Hadiyth kadhaa zimethibiti, mfano zifuatazo:

 

Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba alimuomba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amuombee mama yake hidaaya aingie Uislamu.

 

كُنْتُ أَدْعُو أُمِّي إِلَى الإسلام وَهِيَ مُشْرِكَةٌ، فَدَعَوْتُهَا يَوْمًا فَأَسْمَعَتْنِي فِي رَسُولِ اللَّهِ  صلى الله عليه وسلم مَا أَكْرَهُ، فَأَتَيْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَأَنَا أَبْكِى قُلْتُ: يَا رَسُولَ اللَّهِ، إِنِّي كُنْتُ أَدْعُو أُمِّي إِلَى الإِسْلاَمِ فَتَأْبَى عَلَيَّ فَدَعَوْتُهَا الْيَوْمَ فَأَسْمَعَتْنِي فِيكَ مَا أَكْرَهُ، فَادْعُ اللَّهَ أَنْ يَهْدِىَ أُمَّ أَبِي هُرَيْرَةَ ، فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((اللَّهُمَّ اهْدِ أُمَّ أَبِي هُرَيْرَةَ)) فَخَرَجْتُ مُسْتَبْشِرًا بِدَعْوَةِ نَبِيِّ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم، فَلَمَّا جِئْتُ فَصِرْتُ إِلَى الْبَابِ فَإِذَا هُوَ مُجَافٌ، فَسَمِعَتْ أُمِّي خَشْفَ قَدَمَيَّ فَقَالَتْ: مَكَانَكَ يَا أَبَا هُرَيْرَةَ! وَسَمِعْتُ خَضْخَضَةَ الْمَاءِ قَالَ: فَاغْتَسَلَتْ وَلَبِسَتْ دِرْعَهَا وَعَجِلَتْ عَنْ خِمَارِهَا فَفَتَحَتِ الْبَابَ ثُمَّ قَالَتْ: يَا أَبَا هُرَيْرَةَ ، أَشْهَدُ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَأَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ، قَالَ: فَرَجَعْتُ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَأَتَيْتُهُ وَأَنَا أَبْكِي مِنَ الْفَرَحِ ، قَالَ: قُلْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ أَبْشِرْ! قَدِ اسْتَجَابَ اللَّهُ دَعْوَتَكَ وَهَدَى أُمَّ أَبِى هُرَيْرَةَ! فَحَمِدَ اللَّهَ وَأَثْنَى عَلَيْهِ وَقَالَ خَيْرًا

“Nilikuwa namlingania mama yangu ambaye alikuwa mshirikina, ili aingie Uislamu. Siku moja nilipokuwa namlingania akanifanya nisikie (aliyotamka maovu) kuhusu Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ambayo nilichukia. Nikamwendea huku nikilia. Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika nilikuwa namlingania mama yangu, lakini leo kanifanya nisikie aliyoyasema kuhusu wewe ambayo nimeyachukia, basi muombe Allaah Amhidi mama wa Abiy Hurayrah”. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuombea: ((Ee Allaah, Mhidi mama yake Abuu Hurayrah)). Nikatoka nikiwa na furaha kwa du’aa ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Nilipofika mlangoni nilikuta umefungwa, na mama yangu aliposikia sauti za nyayo zangu, akasema: “Bakia hapo hapo ee Abuu Hurayrah!. Nikasikia mmwagiko wa maji, alipomaliza kuoga na kuvaa nguo yake, akaharakiza kuvaa khimaar yake, akaja kufungua mlango akasema: “Ash-hadu allaa ilaaha illa Allaah wa ash-hadu anna Muhammadan ‘abduhu wa Rasuwluhu – nashuhudia kwamba hakuna muabudiwa wa haki isipokuwa Allaah, na kwamba Muhammad ni mja Wake na Rasuli Wake”.  Hapo nikarudi kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) huku nikilia kwa furaha”. “Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Nakubashiria, Allaah Ameshatakabali du’aa yako na Amemhidi Mama wa Abuu Hurayrah. Akamhimidi Allaah na akamtukuza kisha akasema ya khayr”. [Muslim (4/1938)] 

 

Vile vile pale Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipoomba mmoja kati ya Maquraysh wawili aingie Uislamu.

 

اللهم أَعِزَّ الإسلامَ بأَحَبِّ هذين الرجُلَيْنِ إليك بأبي جهلٍ أو بعمرَ بنِ الخطابِ قال وكان أَحَبَّهُما إليه عمرُ

((Ee Allaah, utie nguvu Uislamu kwa mmojawapo Umpendaye zaidi; Abuu Jahl au ‘Umar bin Al-Khatwaab. Akawa aliyependwa zaidi kati yao ni ‘Umar bin Al-Khattwaab)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (3681)]

 

Pia Imaam Al-Bukhaariy katika mlango wa: “Kuwaombea du’aa washirikina”, Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu):

 

قدِم طُفَيلُ بنُ عمرٍو الدَّوسِيُّ وأصحابُه، على النبيِّ صلَّى اللهُ عليه وسلَّم فقالوا: يا رسولَ اللهِ، إنَّ دَوسًا عصَتْ وأبَتْ، فادْعُ اللهَ عليها، فقيل: هلَكَتْ دَوسٌ، قال: ((اللهمَّ اهدِ دَوسًا وأَتِ بهم))

Atw-Twufayl ibn ‘Amr Ad-Dawsiyy na wenzake walimwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakasema: “(Kabila la) Daws wameasi na wamekanusha (Uislamu). Basi waombee dhidi yao kwa Allaah”. Ikasemwa: “Wameangamia Daws!”  (Lakini Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Akaomba: ((Ee Allaah wahidi Ad-Daws na walete hapa.)) [Al-Bukhaariy (2937), Muslim 2524)]

 

Ama kuhusu kuwaombea Rahmah ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) kauli iliyo na nguvu kabisa ya ‘Ulamaa ni kwamba haifai kuwaombea wasio Waislamu Rahmah, na dalili ni Hadiyth ifuatayo ya Abuu Muwsaa Al-Ash’ariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu):

 

كان اليهودُ يتعاطسون عندَ النبيِّ صلَّى اللهُ عليه وسلَّمَ يرجونَ أنْ يقولَ لهم يرحَمُكم اللهُ فيقولُ يَهْدِيكم اللهُ ، ويُصْلِحُ بالَكُمْ

Mayahudi walikuwa wakipiga chafya (wakichemua) mbele ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakitaraji awaambie: Yarhamukumu-Allaah (Allaah Akurehemuni) lakini husema: ((Yahdiykumu-Allaahu wa Yuswlihu Baalakum (Akuongozeni Allaah na Akutengenezeeni mambo yenu)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (2739)]

 

Pia haifai kuwaombea maghfirah kwa kauli iliyo na nguvu kabisa baina ya ‘Ulamaa.

 

Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema: “Kuwaombea makafiri maghfirah hairuhusiwi kutokana na dalili za Qur-aan na Sunnah and Ijmaa’a ya Ulamaa” [Majmuw’ Al-Fataawaa (12/489)]

 

Na wakiwa wameshafariki haipasi kuwaombea jema lolote. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Amekataza hayo:

 

مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَن يَسْتَغْفِرُوا لِلْمُشْرِكِينَ وَلَوْ كَانُوا أُولِي قُرْبَىٰ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمْ أَنَّهُمْ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ﴿١١٣﴾

Haimpasi Nabiy na wale walioamini kuwaombea maghfirah washirikina japokuwa ni jamaa zao wa karibu baada ya kuwabainikia kwamba wao ni watu wa moto uwakao vikali mno.

 

 

وَمَا كَانَ اسْتِغْفَارُ إِبْرَاهِيمَ لِأَبِيهِ إِلَّا عَن مَّوْعِدَةٍ وَعَدَهَا إِيَّاهُ فَلَمَّا تَبَيَّنَ لَهُ أَنَّهُ عَدُوٌّ لِّلَّـهِ تَبَرَّأَ مِنْهُ ۚ إِنَّ إِبْرَاهِيمَ لَأَوَّاهٌ حَلِيمٌ ﴿١١٤﴾

Na haikuwa Ibraahiym kumuombea maghfirah baba yake isipokuwa kwa sababu ya ahadi aliyoahidiana naye. Lakini ilipombainikia kwamba yeye ni adui wa Allaah, alijiepusha naye. Hakika Ibraahiym ni mwenye huruma mno na mvumilivu. [At-Tawbah: 113- 114]

 

 

Pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((اسْتَأْذَنْتُ رَبِّي أَنْ أَسْتَغْفِرَ لأُمِّي فَلَمْ يَأْذَنْ لِي، وَاسْتَأْذَنْتُهُ أَنْ أَزُورَ قَبْرَهَا فَأَذِنَ لِي))

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Nilimuomba idhini Rabb wangu nimuombee maghfirah mama yangu, Hakunipa idhini. Nikaomba idhini kuzuru kaburi lake Akanipa idhini.)) [Muslim (976)]

 

Imaam An-Nawawiy (Rahimahu Allaah) amesema: “Kumswalia kafiri Swalaah ya janaazah au kumuombea maghfirah ni haram kutokana na nukuu za Qur-aan na Ijmaa’a ya ‘Ulamaa” [Al-Majmuw’ (5/19)]

 

 

 

4- Kuomba Du’aa Jambo Kubwa Na Dogo La Manufaa ya Dunia

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: “Hakuna ubaya kuomba jambo linalohusiana na mambo ya kidunia mfano mtu aseme: “Ee Allaah niruzuku nyumba pana”. Au “Ee Allaah niruzuku mke mzuri”. Au, “Ee Allaah, niruzuku mali nyingi”. Au, “Ee Allaah niruzuku gari zuri”. Hivyo kwa sababu du’aa ni ‘ibaadah hata kama ni kuhusu mambo ya dunia, kwani binaadamu hana kimbilio isipokuwa kwa Allaah”. [Ash-Sharh Al-Mumti’ (3/284)] 

 

 

 

Share