06 - Mambo ya Haramu Kwa Vinyozi: Kufanya Matendo Kinyume Na Urijali

Mambo ya Haramu yanayofanyika katika kazi ya Unyozi:

 

6. Mengine Katika Hizo Kazi Za Unyoaji Hupelekea Vinyozi Wengi Kufanya Matendo Kinyume Na Urijali

 

Katika misiba iliyopo kwa vinyozi hao wenye kutumbukia kwenye haramu hizo, katika hiyo kazi ya kunyoa ndevu za wanaume, kunafikia hadi wakageuka kama wanawake. Maeneo mengi, vinyozi baada ya kumaliza kumnyoa mwanaume ndevu, humpaka aidha majimaji ya marashi yenye kuwasha yajulikanayo kama “after shave” au humpaka poda! Na katika upakaji huo anampapasa kidevu na mashavu na kumsugua kama anamfanyia “massage”!

Hali hiyo inakwenda kinyume na urijali, mwanamme hapaswi kuwa hivyo kabisa!! Si kazi ya kiume hiyo, na isitoshe tayari mwanzo kushapatikana uharamu wa kunyoa ndevu! Allaahul-Musta’aan.

 

Share